bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Thessalonians 5
1 Thessalonians 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
1
Wandugu, si lazima kwenu niwaandikie jambo lolote juu ya wakati wala saa ambayo mambo hayo yatatokea.
2
Kwa maana munajua ninyi wenyewe kwamba siku Bwana atakaporudia, itatimia kwa saa musiyozania kama vile mwizi anavyokuja usiku.
3
Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.
4
Lakini ninyi wandugu, hamuko katika giza, kwa hiyo siku ile haitawafikia kwa rafla kama mwizi.
5
Kwa maana ninyi wote ni watu wanaoishi katika mwangaza, ndio watu wa muchana. Sisi si watu wa usiku wala wa giza.
6
Basi tusilale usingizi kama vile wengine, lakini tukeshe na kuwa wakadirifu.
7
Kwa maana wale wanaolala usingizi wanalala usiku, na wale wanaolewa, wanalewa usiku.
8
Lakini sisi ni watu wa muchana, tunapaswa kuwa wakadirifu. Tunapaswa kushikamana na imani na upendo kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua, nalo tumaini letu la wokovu kama vile kofia ya kutulinda.
9
Kwa maana Mungu hakututayarishia kuangamizwa kwa ukali wa kasirani yake, lakini kuokolewa kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
10
Yeye alikufa kwa ajili yetu, kusudi hata ikiwa tuko wazima au tumekufa, tupate kuishi pamoja naye wakati atakaporudia.
11
Basi mufarijiane na kujengana imani, kama vile munavyozoea kufanya.
12
Wandugu, tunawaomba muwaheshimu sana wale wanaoshugulika na kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwaonya.
13
Muwape heshima kubwa na kuwapenda kwa ajili ya kazi yao. Mukuwe na amani kati yenu.
14
Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.
15
Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
16
Mukuwe na furaha siku zote.
17
Muombe bila kuchoka.
18
Mumushukuru Mungu katika mambo yote. Kwa maana hayo ndiyo mambo Mungu anayotaka mufanye katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.
19
Musizuize kazi ya Roho Mutakatifu.
20
Musizarau ujumbe unaotoka kwa Mungu.
21
Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.
22
Muepuke ubaya wa kila namna.
23
Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.
24
Yule anayewaita ninyi atatimiza mambo hayo, kwa maana yeye ni mwaminifu.
25
Wandugu, mutuombee vilevile.
26
Musalimiane kwa upendo wa kikristo.
27
Ninawasihi kwa jina la Bwana, musome barua hii kwa wandugu wote.
28
Tunawatakia neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
All chapters:
1
2
3
4
5