bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Exodus 37
Exodus 37
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 36
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 38 →
1
Bezaleli akatengeneza sanduku kwa mbao za mujohoro. Urefu wake ulikuwa sentimetre mia moja na kumi, upana sentimetre makumi sita na sita, na urefu kwenda juu sentimetre makumi sita na sita.
2
Akalipakaa zahabu safi ndani na inje na kulifanyia ukingo wa zahabu pande zote.
3
Kisha akatengeneza pete ine za zahabu za kulibebea, akazitia kwenye pembe zake, kila pembe pete moja.
4
Akatengeneza miti ya mujohoro na kuipakaa zahabu.
5
Miti hiyo akaipitisha katika zile pete zinazokuwa katika pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibebea.
6
Akatengeneza kiti cha rehema cha zahabu safi; urefu wake sentimetre mia moja na kumi na upana wake sentimetre makumi sita na sita.
7
Akatengeneza vilevile makerubi wawili kwa kufua zahabu kwenye miisho ya kifuniko hicho;
8
kerubi mumoja mwisho huu na mwingine mwisho mwingine. Akatengeneza makerubi wale kwenye miisho ya kifuniko hicho, wakikuwa kitu kimoja na kifuniko.
9
Makerubi wale walikuwa wakielekeana, mabawa yao yakikunjuliwa na kukifunika kifuniko cha sanduku, nyuso zao zilikielekea kifuniko cha sanduku.
10
Vilevile akatengeneza meza ya mujohoro yenye urefu wa sentimetre makumi nane na nane, upana sentimetre makumi ine na ine, na urefu kwenda juu sentimetre makumi sita na sita.
11
Akapakaa zahabu safi na kuitengenezea ukingo wa zahabu.
12
Akaizungushia ubao wenye upana wa milimetre makumi saba na tano, na kuifanyia ukingo wa zahabu.
13
Akaitengenezea pete ine za zahabu na kuzitia katika pembe zake ine pahali miguu ilipoishia.
14
Pete hizo za kushikilia ile miti ya kuibebea ziliwekwa karibu na ule muzunguko wa ubao.
15
Akatengeneza miti miwili ya mujohoro ya kuibebea, akaipakaa zahabu.
16
Akatengeneza vyombo vya zahabu safi vya kuweka juu ya meza: sahani zake na visahani kwa ajili ya ubani, na bilauri zake na bakuli kwa ajili ya sadaka za kinywaji.
17
Akatengeneza vilevile kinara cha taa kwa zahabu safi. Tako lake na muti wa hicho kinara ulikuwa kitu kimoja pamoja na vikombe vyake, vifundo vyake na maua yake.
18
Matawi sita yalitokeza kila upande wa muti wake, matawi matatu upande mumoja na matawi matatu upande mwingine.
19
Katika kila tawi kulikuwa vikombe vitatu mufano wa maua ya lozi, kila kimoja na kifundo chake na ua lake.
20
Na katika muti kulikuwa vikombe vine mufano wa maua ya lozi, pamoja na vifundo vyake na maua yake.
21
Kulikuwa kifundo kila pahali matawi mawilimawili yalipotokea kufuatana na yale matawi sita yanayotoka kwa kile kinara.
22
Vifundo hivyo na matawi vilikuwa kitu kimoja na kinara hicho na chote kilifuliwa kwa zahabu safi.
23
Akatengeneza taa zake saba, koleo zake na visahani vyake kwa zahabu safi.
24
Akatengeneza kinara hicho na vifaa vyake kwa kilo makumi tatu na tano za zahabu.
25
Akatengeneza mazabahu ya kufukizia ubani kwa mbao za mujohoro. Mazabahu hiyo ilikuwa ya muraba, sentimetre makumi ine na tano kwa sentimetre makumi ine na tano, na urefu kwenda juu sentimetre makumi tisa. Pembe za mazabahu hiyo zilikuwa kitu kimoja na mazabahu yenyewe.
26
Yote aliipakaa zahabu safi: upande wake wa juu, pande zake za ubavu na pembe zake. Vilevile akaitengenezea ukingo wa zahabu.
27
Akatengeneza pete mbili za zahabu chini ya ukingo kwenye pande mbili zinazoelekeana. Pete hizo zilitumika kushikilia miti ya kuibebea.
28
Akafanya miti miwili ya mujohoro na kuipakaa zahabu.
29
Akatengeneza mafuta matakatifu ya kupakaa na ubani safi wenye harufu nzuri uliochanganywa vizuri kama manukato.
← Chapter 36
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 38 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40