bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Luke 3
Luke 3
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 4 →
1
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,
2
nao Anasi na Kayafa walikuwa Makuhani Wakubwa. Halafu Mungu akatoa ujumbe wake kwa Yoane mwana wa Zakaria katika jangwa.
3
Basi Yoane akapita katika inchi zote zinazokuwa pembeni ya muto Yordani, akihubiri. Akawaambia watu wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawaondolea zambi.
4
Hivi yakatimia maneno haya yaliyoandikwa katika kitabu cha maneno ya nabii Isaya: “Sauti inatangaza katika jangwa: ‘Mutengeneze njia ya Bwana, munyooshe pahali atakapopita!
5
Hivi kila bonde litafunikwa. Kila mulima na kila kilima vitasawanishwa. Njia zenye lukumba zitanyooshwa, nazo njia zenye mashimo zitalainishwa.
6
Kila mutu ataona jinsi Mungu atakavyotuokoa.’ ”
7
Halafu watu wengi walimufikia Yoane kusudi awabatize. Naye aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliwaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?
8
Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Musianze tu kujisemesha kwamba Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!
9
Hata sasa shoka limekwisha kuwekwa tayari kwenye mashina ya miti. Kila muti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.”
10
Halafu watu wale wakamwuliza: “Basi tufanye nini?”
11
Naye akawajibu: “Mwenye kuwa na kanzu mbili atoe moja kwa yule asiyekuwa na kitu, na anayekuwa na vyakula afanye hivi vilevile.”
12
Walipishaji wa kodi nao wakamufikia vilevile kusudi wabatizwe. Wakamwuliza: “Mwalimu, tufanye nini?”
13
Naye akawajibu: “Musilipishe zaidi kuliko vile inavyoamuriwa.”
14
Nao waaskari wakamwuliza: “Na sisi, tufanye nini?” Naye akawajibu: “Musifanye ukorofi kwa mutu yeyote wala kumusingizia mutu, lakini mutoshelewe na mishahara yenu.”
15
Watu walikuwa wakitazamia kuja kwa Kristo, na wote wakazania kwamba labda Yoane ndiye yeye.
16
Basi Yoane akawaambia wote: “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yule atakayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto.
17
Anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”
18
Na Yoane aliwahubiria watu wale Habari Njema akiwatolea maonyo mengi mbalimbali.
19
Yoane alimukaripia mutawala Herode juu ya kumwoa Herodia, muke wa ndugu yake Filipo na juu ya mabaya mengine.
20
Lakini Herode akaongeza ubaya mwingine kwa kumutia Yoane ndani ya kifungo.
21
Watu wale wote walipobatizwa, Yesu akabatizwa vilevile. Alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka,
22
na Roho Mutakatifu akashuka juu yake katika hali ya kimwili kwa mufano wa njiwa. Na sauti ikasikilika toka mbinguni ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24