bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Mark 1
Mark 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 2 →
1
Huu ndio mwanzo wa Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2
Na imeandikwa hivi katika kitabu cha nabii Isaya: “Mungu anasema: ‘Ninamutuma mujumbe wangu akutangulie, kusudi akutengenezee njia.’
3
Sauti inatangaza katika jangwa: ‘Mutengeneze njia ya Bwana, munyooshe pahali atakapopita!’ ”
4
Hivi Yoane alitokea katika jangwa, akibatiza watu, akiwahubiri kwamba wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawasamehe.
5
Watu wengi walitoka katika Yerusalema na katika jimbo lote la Yudea kwa kumwendea Yoane. Walikubali zambi zao, naye akawabatiza katika muto Yordani.
6
Yoane alikuwa akivaa nguo iliyotengenezwa na manyoya ya ngamia na mukaba wa ngozi katika kiuno. Naye alikuwa akikula nzige na asali ya pori.
7
Yeye alihubiri hivi kwa watu: “Yule anayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kuinama na kufungua kamba ya viatu vyake.
8
Mimi nimewabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu.”
9
Katika siku zile, Yesu akatoka Nazareti, katika Galilaya, akabatizwa na Yoane katika Yordani.
10
Mara moja wakati Yesu alipotoka ndani ya maji, akaona mbingu zinafunguka na Roho Mutakatifu akishuka juu yake kwa mufano wa njiwa.
11
Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”
12
Kisha Roho Mutakatifu akamusukuma Yesu kwenda katika jangwa.
13
Akabaki katika jangwa kwa muda wa siku makumi ine, na kule Shetani akamujaribu. Alikaa kule katikati ya nyama wa pori, nao wamalaika walimushugulikia.
14
Nyuma ya kutiwa kwa Yoane katika kifungo, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema inayotoka kwa Mungu.
15
Alisema: “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu ni karibu! Mugeuke toka zambi zenu na kukubali Habari Njema!”
16
Wakati Yesu alipokuwa akitembea pembeni ya ziwa la Galilaya akawaona wavuvi wawili, waliokuwa wandugu za tumbo: Simoni na ndugu yake Andrea. Walikuwa wakitupa nyavu katika ziwa lile.
17
Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”
18
Mara moja wakaacha nyavu zao na kumufuata.
19
Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili: Yakobo na Yoane waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo wakitengeneza nyavu zao.
20
Mara moja akawaita. Basi wakamwacha baba yao Zebedayo ndani ya chombo pamoja na watumishi wake, wakamufuata Yesu.
21
Yesu na wanafunzi wake walienda Kapernaumu. Siku ya Sabato ilipotimia, Yesu akaingia katika nyumba ya kuabudia na kufundisha watu.
22
Watu waliomusikia walishangaa sana kuona namna alivyofundisha, kwa maana hakuwafundisha sawa na walimu wao wa Sheria, lakini kama mutu mwenye mamlaka.
23
Saa ile, mutu mumoja aliyeshikwa na pepo alikuwa ndani ya nyumba ya kuabudia. Akaanza kulalamika, akisema:
24
“Kuna maneno gani kati yako na sisi, wewe Yesu wa Nazareti? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani: wewe ni Mutakatifu aliyetumwa na Mungu.”
25
Yesu akamukaripia kwa nguvu, akimwamuru: “Nyamaza, na utoke ndani ya mutu huyu!”
26
Yule pepo akamutikisa mutu yule kwa nguvu, akatoka ndani yake, akilalamika kwa nguvu.
27
Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”
28
Halafu sifa za Yesu zikaenea upesi katika jimbo lote la Galilaya.
29
Yesu na wanafunzi wake walipotoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, mara moja wakaenda kwa nyumba ya Simoni na Andrea, wakiwa pamoja na Yakobo na Yoane.
30
Mama mukwe wa Simoni alikuwa katika kitanda, kwa sababu alikuwa na homa. Wakati Yesu alipofika pale, mara moja wakamupasha habari ya ugonjwa wake.
31
Basi Yesu akajongea karibu naye, akamushika mukono na kumusimamisha. Naye akapona homa na kuanza kuwashugulikia.
32
Ilipokuwa magaribi, jua lilipokuwa limekwisha kutua, wakamuletea Yesu watu wote waliokuwa wagonjwa na waliokuwa na pepo.
33
Watu wote wa muji walikusanyika mbele ya mulango wa nyumba.
34
Yesu akawaponyesha watu wengi wenye magonjwa mbalimbali. Vilevile alifukuza pepo wengi, wala hakuwaachilia pepo kusema neno, kwa sababu walimujua yeye ni nani.
35
Kesho yake asubui kulipokuwa kungali giza, Yesu akaamuka, akatoka katika muji na kwenda pahali penye ukiwa, kule akaanza kuomba.
36
Basi Simoni na wenzake wakaenda kumutafuta.
37
Nao walipomwona wakamwambia: “Watu wote wanakutafuta.”
38
Lakini Yesu akawajibu: “Twende pahali pengine katika vijiji vinavyokuwa karibu, kusudi nihubiri kule vilevile, kwa maana ni kwa ajili ya ile nimekuja.”
39
Hivi akaenda fasi zote katika Galilaya, akihubiri katika nyumba za kuabudia na kufukuza pepo.
40
Mutu mumoja mwenye ukoma alikuja kwa Yesu, akapiga magoti mbele yake na kumusihi, akisema: “Kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”
41
Yesu akamusikilia huruma, akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka utakaswe!”
42
Na mara moja mutu yule akapona ukoma na kutakaswa.
43
Pale pale Yesu akamwagiza kwa nguvu aende na kusema:
44
“Angalisho, usimwambie mutu hata neno moja juu ya hii. Lakini kwenda kwa kuhani na kumwonyesha jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa wote kwamba umetakaswa.”
45
Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16