bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Numbers 1
Numbers 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 2 →
1
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:
2
Wewe na Haruni mufanye hesabu ya Waisraeli wote na kuandika majina ya wanaume wote, kulingana na ukoo na jamaa zao.
3
Wale wote katika Israeli wanaoweza kwenda kwa vita, wenye umri kuanzia miaka makumi mbili na zaidi, mutawaweka katika hesabu ya majeshi yao.
4
Kiongozi mumoja wa jamaa kutoka kila kabila atakusaidia kufanya hesabu.
5
Haya ni majina ya watu watakaokusaidia: Kabila la Rubeni: Elisuri mwana wa Sedeuri; Kabila la Simeoni: Selumieli mwana wa Suri-Sadai; Kabila la Yuda: Nasoni mwana wa Aminadabu; Kabila la Isakari: Netaneli mwana wa Suari; Kabila la Zebuluni: Eliabu mwana wa Heloni; Kabila la Efuraimu: Elisama mwana wa Amihudi; Kabila la Manase: Gamalieli mwana wa Pedasuri; Kabila la Benjamina: Abidani mwana wa Gideoni; Kabila la Dani: Ahiezeri mwana wa Amishadai; Kabila la Aseri: Pagieli mwana wa Okrani; Kabila la Gadi: Eliasafu mwana wa Deueli; Kabila la Nafutali: Ahira mwana wa Enani.
6
Hao viongozi waliochaguliwa kati ya watu wa Israeli walikuwa vilevile viongozi wa jeshi.
7
Basi, Musa na Haruni wakawatwaa watu hao waliotajwa.
8
Na katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, wakakusanya Waisraeli wote. Waliandika majina ya wote wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi, kulingana na jamaa zao na ukoo zao,
9
kama vile Yawe alivyomwamuru Musa. Musa akawahesabu watu hawa kule katika jangwa la Sinai.
10
Kwa kila kabila la Israeli, walihesabu watu kulingana na jamaa zao na ukoo zao. Waliandika majina ya kila mwanaume aliyekuwa na umri wa miaka makumi mbili na zaidi, aliyefaa kuingia katika jeshi. Hii ni hesabu yao kulingana na kabila yao. Kabila la Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli: elfu makumi ine na sita na mia tano. Kabila la Simeoni: elfu makumi tano na tisa na mia tatu. Kabila la Gadi: elfu makumi ine na tano mia sita na makumi tano. Kabila la Yuda: elfu makumi saba na ine na mia sita. Kabila la Isakari: elfu makumi tano na ine na mia ine. Kabila la Zebuluni: elfu makumi tano na saba mia ine. Kabila la Efuraimu: elfu makumi ine na mia tano. Kabila la Manase: elfu makumi tatu na mbili na mia mbili. Kabila la Benjamina: elfu makumi tatu na tano na mia ine. Kabila la Dani: elfu makumi sita na mbili na mia saba. Kabila la Aseri: elfu makumi ine na mumoja na mia tano. Kabila la Nafutali: elfu makumi tano na tatu na mia nane.
11
Hao ndio watu waliokuwa wamehesabiwa ambao Musa na Haruni waliwahesabu wakisaidiwa na wale viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila kiongozi akisimamia ukoo wake. 45Hivyo jumla ya wanaume wote wa Israeli wenye umri kuanzia miaka makumi mbili na zaidi, waliofaa kuingia katika jeshi katika inchi ya Israeli, 46ilikuwa watu elfu mia sita na tatu na mia tano makumi tano. 47Lakini Walawi hawakuhesabiwa pamoja na yale makabila mengine, 48kwa sababu Yawe alimwambia Musa: 49Usifanye hesabu ya kabila la Lawi pamoja na ile ya watu wa Israeli. 50Utawachagua wakuwe waangalizi wa hema la kuchunga vibao vya agano, vyombo vyake vyote na kila kitu kinachokuwa ndani yake; watakuwa wakilibeba pamoja na vyombo vyake vyote. Watatumika mule ndani na watapiga kambi yao kwa kulizunguka. 51Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa. 52Waisraeli wengine wote watapiga kambi zao makundi makundi, kila mutu katika kundi lake na chini ya bendera yake. 53Lakini Walawi watapiga kambi zao kuzunguka hema la kuchunga vibao vya agano kusudi walilinde na kasirani yangu isiwake juu ya Waisraeli. 54Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36