bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
/
John 6
John 6
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 7 →
1
BAADA ya haya Yesu alikwenda zake ngʼambu ya bahari ya Galilaya, bahari ya Tiberia.
2
Makutano mengi wakamfuata, kwa sababu waliziona ishara alizowafanyia wagonjwa.
3
Yesu akapanda mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
4
Na Pasaka, siku kuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu.
5
Bassi Yesu alipoinua macho yake akaona makutano mengi yanakuja kwake, akamwambia Filipo, Tununue wapi mikate, hawa wapate kula?
6
Alinena haya illi amjaribu: kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda.
7
Filipo akamjibu, Mikate ya dinari miateen haiwatoshi, killa mmoja apate kidogo tu.
8
Mmoja wa wanafunzi wake, Andrea, ndugu wa Simon Petro, akamwambia,
9
Yupo mtoto hapa, ana mikate mitano ya shayiri na samaki wawili, lakini haya nini kwa watu wengi kama hivi?
10
Yesu akasema, Waketisheni watu. Palikuwako majani tele mahali pale. Bassi watu waume wakaketi, jumla yao wapata elfu tano.
11
Bassi Yesu akaitwaa mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.
12
Waliposhiba, akawaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kitu kisipotee.
13
Bassi wakavikusanya, wakajaza vikapu thenashara kwa vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia waliokula.
14
Bassi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya Yesu, wakasema, Huyu hakika ni nabii yule ajae ulimwenguni.
15
Bassi Yesu, akitambua ya kuwa walitaka kuja kumchukua illi wamfanye mfalme, akajitenga, akaenda tena mlimani, yeye peke yake.
16
Hatta ilipokuwa jioni, wanafunzi wake wakatelemka baharini:
17
wakapanda chomboni wakaanza kuivuka bahari kwenda Kapernaum. Na giza imekwisha kuwa, nae Yesu hajawafikia.
18
Bahari ikaanza kuchafuka, upepo mwingi ukivuma.
19
Bassi wakavuta makasia kadiri ya stadio ishirini na tano au thelathini, wakamwona Yesu anakwenda juu ya bahari, anakikaribia chombo: wakaogopa.
20
Nae akawaambia. Ni mimi, msiogope.
21
Bassi wakataka kumpokea chomboni; na marra hiyo chombo kikaifikilia inchi waliyokuwa wakienda.
22
Siku ya pili yake makutano waliosimama ngʼambu ya bahari wakaona ya kuwa hakuna mashua nyingine huko illa ile moja waliyoingia wanafunzi wake; tena ya kuwa Yesu hakuingia katika mashua ile pamoja na wanafunzi wake, bali wanafunzi wake walikwenda peke yao,
23
(lakini mashua nyingine zilikuja kutoka Tiberia karibu na pahali pale walipokula mikate, wakati Bwana aiiposhukuru);
24
bassi makutano walipoona ya kuwa Yesu hakuwako huko wala wanafunzi wake, wenyewe wakaingla vyomboni, wakaenda Kapernaum wakimtafuta Yesu.
25
Hatta walipomwona ngʼambu ya bahari, wakamwambia, Rabbi, umekuja lini hapa?
26
Yesu akawajibu, akasema, Amin, amin, nawaambieni, Mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate, mkashiba.
27
Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hatta uzima wa milele, Mwana wa Adamu atakachowapeni: maana huyu ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu.
28
Bassi wakamwambia, Tufanyeje tupate kuzitenda kazi za Mungu?
29
Yesu akajibu, akawaambia, Hii ni kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa nae.
30
Wakamwambia, Unafanya ishara gani bassi illi tuone tukaamini? Unatenda kazi gani?
31
Baba zetu waliila manna jangwani, kama ilivyoandikwa, Aliwapa mkate kutoka mbinguni wale.
32
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa mkate ule kutoka mbinguni, bali Baba yangu anawapa mkate ule utokao mbinguni ulio wa kweli.
33
Kwa maana mkate wa Mungu ni ule ushukao kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.
34
Bassi, wakamwambia, Bwana, siku zote utupe mkate huo.
35
Yesu akawaambia, Mimi ni mkate wa uzima; yeye ajae kwangu hataona njaa kabisa, nae aniaminiye hataona kiu kamwe.
36
Lakini naliwaambieni ya kwamba mmeniona bila kuniamini.
37
Yote anipayo Bwana itakuja kwangu; nae ajae kwangu sitamtupa nje kamwe.
38
Kwa kuwa sikushuka kutoka mbinguni illi niyafanye mapenzi yangu, hali mapenzi yake aliyenipeleka.
39
Na mapenzi yake Baba aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika vyote alivyonipa nisipoteze kitu hatta kimoja, hali nikifufue siku ya mwisho.
40
Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya ya kwamba killa amtazamae Mwana na kumwamini awe ua uzima wa milele, nami nitamfufua siku ya mwisho.
41
Bassi Wayahudi wakamnungʼunikia, kwa sababu alisema, Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni.
42
Wakanena, Huyu siye Yesu, mwana wa Yusuf, ambae twamjua baba yake na mama yake? Bassi, anenaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?
43
Bassi Yesu akajibu, akawaambia, Msinungʼunike ninyi kwa ninyi.
44
Hakuna mtu awezae kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka: nami nitamfufua siku ya mwisho.
45
Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Bassi killa aliyesikia na kujifunza kwa Baba, huja kwangu.
46
Si kwamba mtu amemwona Baba, illa yeye atokae kwa Mungu huyu ndiye aliyemwona Baba.
47
Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi ana uzima wa milele.
48
Mimi ni mkate wa uzima.
49
Baba zetu waliila manna jangwani wakafa.
50
Huu ni mkate ushukao kutoka mbinguni, illi mtu aule wala asife.
51
Mimi ni mkate wa uzima ulioshuka kutoka mbinguni; mtu akila mkate huu, ataishi milele: na mkate nitakaotoa mimi ni nyama yangu nitakayotoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.
52
Bassi Wayahudi wakashindana wao kwa wao, wakinena; Awezaje mtu huyu kutupa sisi nyama yake tuile?
53
Bassi Yesu akawaambia, Amin, amin, nsiwaambieni. Msipoila nyama yake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani jemi.
54
Ailae nyama yangu na kuinywa damu yangu ana uzima wa milele; mimi nitamfufua siku ya mwisho.
55
Kwa maima nyama yangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli,
56
Ailae nyama yangu na kuinywa damu yangu, hukaa ndani yangu, na mimi ndani yake.
57
Kama vile Baba aishiye alivyonituma mimi, nami naishi kwa ajili ya Baba, kadhalika yeye nae anilae ataishi kwa ajili yangu.
58
Huu ni mkale ulioshuka kutoka mbinguni; si kama baba zenu walivyoila manna wakafa; aulae mkate huu ataishi milele.
59
Maneno haya aliyasema sunagogini, alipokuwa akifundisha huko Kapenaum.
60
Bassi watu wengi katika wanafunzi wake waliposikia haya, wakasema, Neno hili ni gumu, nani awezae kulisikia?
61
Yesu akajua nafsini mwake ya kuwa wanafunzi wake wanaliumigʼunikia neno hili, akawaambia, Neno hili linawachukiza?
62
Itakuwaje, bassi, mmwonapo Mwana wa Adamu akijianda huko alikokuwa kwanza?
63
Roho ndiyo itiayo uzima; mwili haufai kitu; maneno ninayowaambieni ni roho, tena ni uzima.
64
Lakini kuna wengine miongoni mwemi wasioamini. Maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini na ni nani atakaenisaliti.
65
Akanena, Kwa sababu hii nimewaambia ya kwamba hapana mtu awezae kuja kwangu, isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.
66
Kwa ajili ya haya wengi katika wanafunzi wake wakarejea nyuma, wala hawakuandamana nae tena.
67
Bassi Yesu akawaambia wathenashara, Ninyi nanyi mnataka kuondoka?
68
Bassi Simon Petro akamjibu, Bwana! twende kwa nani? Wewe una maneno ya uzima wa milele.
69
Nasi tumeamini, tena tumejua ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hayi.
70
Yesu akawajibu, Je! sikuwachagua ninyi thenashara, na mmoja wenu ni Shetani?
71
Alimnena Yuda, mwana wa Simon Iskariote: maana huyu ndiye atakaemsaliti: nae ni mmoja wa wathenashara.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21