bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
/
Deuteronomy 15
Deuteronomy 15
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 16 →
1
Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
2
Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Mwenyezi Mungu wa kufuta madeni umetangazwa.
3
Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
4
Hata hivyo, hapatakuwa na maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
5
ikiwa tutamtii Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
6
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
7
Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
8
Bali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
9
Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Mwenyezi Mungu dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
10
Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
11
Siku zote watakuwa watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe wakarimu kwa ndugu zenu walio maskini na wahitaji katika nchi yenu.
12
Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
13
Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
14
Mpe kwa hiari kutoka kundi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka, na kutoka shinikizo lako la kukamulia zabibu. Mpe kama vile Mwenyezi Mungu, Mungu wako, alivyokubariki.
15
Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
16
Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
17
ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake hadi hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mjakazi wako.
18
Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakubariki kwa kila kitu utakachofanya.
19
Wekeni wakfu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ng’ombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
20
Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, pale mahali atakapopachagua.
21
Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.
22
Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote walio najisi na waliotakasika mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
23
Lakini kamwe msile damu; imwageni ardhini kama maji.
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 16 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34