bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
/
Deuteronomy 7
Deuteronomy 7
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 8 →
1
Mwenyezi Mungu, Mungu wako, akuletapo katika nchi unayoingia kuimiliki, na awafukuzapo mbele yako mataifa mengi, yaani Wahiti, Wagirgashi, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, mataifa saba makubwa tena yenye nguvu kuliko wewe,
2
pia Mwenyezi Mungu, Mungu wako, atakapowatia mkononi mwako na ukawashinda, basi ni lazima uwaangamize wote kabisa. Usifanye agano nao, wala usiwahurumie.
3
Usioane nao. Usimtoe binti yako kuolewa na mwanawe, au kumchukua binti yake aolewe na mwanao.
4
Kwa maana watamgeuza mwanao aache kunifuata, ili aitumikia miungu mingine, nayo hasira ya Mwenyezi Mungu itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza ghafula.
5
Hili ndilo utakalowafanyia: Vunja madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia, katakata nguzo zao za Ashera, na kuchoma sanamu zao kwa moto;
6
kwa kuwa wewe ni taifa takatifu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wako. Mwenyezi Mungu, Mungu wako, amekuchagua kutoka mataifa yote duniani uwe taifa lake, hazina yake ya pekee.
7
Mwenyezi Mungu hakuweka upendo wake juu yenu na kuwachagua kwa sababu mlikuwa wengi mno kuliko watu wengine, kwa maana ninyi ndio mliokuwa wachache sana kuliko mataifa yote.
8
Lakini ni kwa sababu Mwenyezi Mungu aliwapenda ninyi na kutunza kiapo alichowaapia babu zenu kwamba atawatoa ninyi kwa mkono wenye nguvu na kuwakomboa kutoka nchi ya utumwa, kutoka nguvu za Farao mfalme wa Misri.
9
Basi ujue kwamba Mwenyezi Mungu, Mungu wako, ndiye Mungu; ni Mungu mwaminifu, anayetunza agano la upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanaompenda na kuzishika amri zake.
10
Lakini kwa wale wanaomchukia atawalipiza kwenye nyuso zao kwa maangamizi; hatachelewa kuwalipiza kwenye nyuso zao wale wamchukiao.
11
Kwa hiyo, kuweni waangalifu kufuata maagizo, amri na sheria ninazowapa leo.
12
Mkizingatia sheria hizi na kuzifuata kwa uangalifu, basi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atatunza agano lake la upendo nanyi, kama alivyowaapia baba zenu.
13
Atawapenda ninyi na kuwabariki na kuongeza idadi yenu. Atabariki uzao wa tumbo lenu, mazao ya nchi yenu, nafaka, divai mpya na mafuta, ndama za ng’ombe wa makundi yenu, na kondoo wa makundi yenu katika nchi ile aliyoapa kuwapa baba zenu.
14
Mtabarikiwa kuliko mataifa mengine yote, hakuna wanaume wala wanawake kwenu watakaokosa watoto, wala mifugo yenu haitakuwa tasa.
15
Mwenyezi Mungu atawakinga na kila ugonjwa. Mungu hatatia juu yenu ugonjwa wowote mbaya mlioufahamu huko Misri, lakini atatia ugonjwa juu ya wale wote wanaokuchukia.
16
Ni lazima mwangamize watu wote ambao Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atawatia mikononi mwenu. Msiwatazame kwa kuwahurumia na msiitumikie miungu yao, kwa kuwa itakuwa mtego kwenu.
17
Mnaweza kujiuliza wenyewe: “Mataifa haya ni yenye nguvu kuliko sisi. Tutawezaje kuwafukuza?”
18
Lakini msiwaogope. Kumbukeni vyema jinsi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, alivyofanya kwa Farao na kwa wote huko Misri.
19
Mliona kwa macho yenu wenyewe majaribu makubwa, ishara za miujiza na maajabu, mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, ambao kwa huo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, aliwatoa mtoke Misri. Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atawafanyia hivyo watu wote ambao mnawaogopa sasa.
20
Zaidi ya hayo, Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atatuma nyigu miongoni mwao hadi yale mabaki watakaojificha waangamie.
21
Msiingiwe na hofu kwa sababu yao, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambaye yupo miongoni mwenu ni mkuu naye ni Mungu wa kutisha.
22
Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atawafukuza mataifa hayo mbele yenu kidogo kidogo. Hamtaruhusiwa kuwaondoa wote kwa mara moja, la sivyo wanyama pori wataongezeka na kuwa karibu nanyi.
23
Lakini Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atawatia watu hao mikononi mwenu, akiwatia katika machafuko makubwa hadi waangamizwe.
24
Atawatia wafalme wao mikononi mwenu, nanyi mtayafuta majina yao chini ya mbingu. Hakuna hata mmoja atakayeweza kusimama dhidi yenu bali mtawaangamiza.
25
Sanamu za miungu yao mtazichoma moto. Msitamani fedha wala dhahabu iliyo juu ya vinyago hivyo, wala msiichukue iwe yenu, la sivyo mtakuwa mmetekwa nayo. Kwa kuwa ni chukizo kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.
26
Msilete vitu vya machukizo katika nyumba zenu kwani ninyi, mtatengwa kama vitu hivyo kwa maangamizi. Ukichukie kabisa kitu hicho kwa kuwa kimetengwa kwa maangamizi.
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 8 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34