bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Kings 13
2 Kings 13
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 14 →
1
Katika mwaka wa makumi mbili na tatu wa utawala wa mufalme Yoasi wa Yuda, Yoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli, akaendelea kutawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka kumi na saba.
2
Alitenda maovu mbele ya Yawe. Alitenda zambi sawa na Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Hakuacha kutenda zambi hii.
3
Yawe alikasirika, akawafanya watu wa Israeli washindwe katika vita mara kwa mara na mufalme Hazaeli wa Aramu na mwana wake Beni-Hadadi.
4
Yoahazi akamusihi Yawe, naye Yawe alipoona jinsi mufalme wa Aramu alivyowatesa watu wa Israeli akasikia maombi yake.
5
Yawe akawapa Waisraeli kiongozi ambaye aliwakomboa kutoka kwa Waaramu. Halafu wakakaa kwa amani kama vile walivyokuwa zamani.
6
Hata hivyo hawakuacha zambi za mufalme Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi; lakini waliendelea na zambi zao na sanamu ya Ashera ilibakia kule Samaria.
7
Yoahazi hakukuwa na waaskari, lakini alikuwa tu na wapanda-farasi makumi tano, magari kumi na waaskari wa miguu elfu kumi. Hii ilikuwa ni kwa sababu mufalme wa Aramu alikuwa ameyaangamiza makundi ya waaskari ya Israeli na kuyakanyaga chini kama mavumbi.
8
Mambo mengine ya Yoahazi, yote aliyofanya na ushujaa wake yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
9
Yoahazi akakufa na kuzikwa kule Samaria, naye mwana wake Yoasi akakuwa mufalme kwa pahali pake.
10
Katika mwaka wa makumi tatu na saba wa utawala wa mufalme Yoasi wa Yuda, Yoasi mwana wa Yoahazi alianza kutawala Israeli akiwa kule Samaria, na akatawala kwa muda wa miaka kumi na sita.
11
Yoasi vilevile alitenda maovu mbele ya Yawe. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliendelea kuzitenda.
12
Mambo mengine ya Yoasi, yote aliyofanya na ushujaa wake katika vita alivyopigana na mufalme Amazia wa Yuda, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
13
Yoasi akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme kule Samaria, naye mwana wake Yeroboamu akatawala kwa pahali pake.
14
Nabii Elisha alipata ugonjwa ambao ulimwua. Alipokuwa karibu kufa, mufalme Yehoasi wa Israeli alimutembelea. Alipomufikia Elisha, akalia, akisema: “Baba yangu, baba yangu! Ulikuwa wa lazima kuliko magari ya Israeli na wapanda-farasi wake!”
15
Elisha akamwamuru: “Ulete upinde na mishale!” Yoasi akavileta.
16
Elisha akamwambia ajitayarishe kupiga mishale. Mufalme akajitayarisha na Elisha akaiweka mikono yake juu ya mikono ya mufalme.
17
Mufalme alifuata maagizo ya nabii na kufungua dirisha ambalo lilielekea Aramu. Elisha akatoa amri: “Tupa mushale!” Mara tu mufalme alipotupa mushale, nabii akasema: “Wewe ndio mushale wa Yawe, ambao kwa njia yake atapata ushindi juu ya Waaramu. Utapigana na Waaramu kule Afeki mpaka uwashinde.”
18
Halafu Elisha akamwambia mufalme atwae mishale mingine na kuipiga chini. Mufalme akapiga mishale chini mara tatu, kisha akaacha.
19
Elisha akakasirika sana, akamwambia mufalme: “Mbona haukupiga mara tano au sita? Hivyo ungewaangamiza Waaramu kabisa. Lakini sasa utawashinda mara tatu tu.”
20
Elisha akakufa, naye akazikwa. Kila mwaka, makundi ya Wamoabu yalikuja kuishambulia inchi ya watu wa Israeli.
21
Siku moja, wakati wa mazishi, watu waliona moja kati ya makundi yale. Wakatupa maiti katika kaburi la Elisha na kukimbia. Mara tu maiti hiyo ilipogusa mifupa ya Elisha, ilifufuka na kusimama wima.
22
Mufalme Hazaeli wa Aramu akawatesa sana watu wa Israeli wakati wote wa utawala wa Yoahazi.
23
Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.
24
Hazaeli mufalme wa Aramu alipokufa, Beni-Hadadi mwana wake akatawala kwa pahali pake.
25
Mufalme Yoasi akamushinda Beni-Hadadi mara tatu na kuikomboa miji yote iliyotekwa wakati wa utawala wa Yoahazi, baba ya Yoasi.
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 14 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25