bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Kings 20
2 Kings 20
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 21 →
1
Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya, mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: “Yawe amesema hivi: ‘Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.’ ”
2
Hezekia akageukia upande wa ukuta na kumwomba Yawe, akisema:
3
“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.
4
Lakini mbele Isaya hajapita kiwanja cha katikati, Yawe akamutolea ujumbe kusema:
5
“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.
6
Nitakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi. Nitakuokoa wewe pamoja na muji huu toka katika mikono ya mufalme wa Asuria. Nitaulinda muji huu kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi.”
7
Basi Isaya akasema: “Mulete mukate wa tini halafu muutwae na kuuweka kwenye jipu lake, kusudi apate kupona.”
8
Hezekia akamwuliza Isaya: “Ni kitambulisho gani ambacho kitanionyesha kwamba kweli Yawe ataniponyesha na katika siku ya tatu nitaweza kwenda kwa nyumba ya Yawe?”
9
Isaya akamujibu: “Hiki kitakuwa kitambulisho kwako kutoka kwa Yawe, kwamba Yawe atafanya kama alivyoahidi: Unataka kivuli kiende hatua kumi mbele au nyuma?”
10
Hezekia akamujibu: “Ni vyepesi zaidi kivuli kwenda mbele hatua kumi! Basi kirudi nyuma hatua kumi.”
11
Isaya akamwomba Yawe, naye Yawe akafanya kivuli kirudi hatua kumi kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi.
12
Wakati ule, mufalme Berodaki-Baladana mwana wa Baladani mufalme wa Babeli alisikia kwamba Hezekia alikuwa amegonjwa na sasa amepona, alimutumia ujumbe pamoja na zawadi.
13
Basi, Hezekia akawakaribisha na kuwaonyesha mali yake: nyumba yake ya hazina, feza, zahabu, viungo vya kukolezea chakula, mafuta ya bei kali na nyumba ya vifaa vyake vyote vya kiaskari na vitu vyote vilivyokuwa katika akiba zake. Hakukukuwa kitu chochote katika nyumba yake, au inchi yake ambacho hakuwaonyesha.
14
Halafu nabii Isaya akamwendea mufalme Hezekia na kumwuliza: “Watu hawa wamesema nini? Na, wamekujia kutoka wapi?” Naye Hezekia akamujibu: “Wamenifikia kutoka inchi ya mbali.”
15
Halafu akamwuliza: “Wameona nini katika nyumba yako?” Hezekia akamujibu: “Wameona yote yanayokuwa katika nyumba yangu. Hakuna kitu chochote katika akiba zangu ambacho sikuwaonyesha.”
16
Halafu Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yawe:
17
Siku zinakuja ambapo vyote vinavyokuwa katika nyumba yako na vitu vyote babu zako walivyokusanya mpaka leo, vitapelekwa Babeli. Hakuna kitu chochote kitakachobaki. –Ni Yawe anayesema hivyo.–
18
Tena wamoja kati ya watoto wako wanaume watapelekwa, nao watakuwa matowashi katika nyumba ya mufalme wa Babeli.”
19
Naye Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yawe ulilosema ni zuri.” Alisema hivyo maana alifikiri: “Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.”
20
Matendo mengine ya Hezekia, ushujaa wake na maelezo juu ya jinsi alivyojenga kisima na kuchimba mufereji wa kuleta maji katika muji, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
21
Hezekia akakufa, naye mwana wake Manase akatawala kwa pahali pake.
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 21 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25