bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jonah 1
Jonah 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 2 →
1
Neno la Yawe lilimufikia Yona mwana wa Amitai kusema hivi:
2
Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uukaripie. Maana uovu wake umenifikia.
3
Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.
4
Lakini Yawe akavumisha upepo mukali katika bahari, kukatokea zoruba kali. Mashua ikakuwa karibu kuvunjika kabisa.
5
Watumishi wa mashua wakaogopa, kila mumoja akaanza kumulilia mungu wake. Wakatupa katika bahari mizigo yote kwa kupunguza uzito wa mashua. Wakati ule, Yona alikuwa ameshuka katika sehemu ya ndani ya mashua, akalala usingizi muzito.
6
Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.
7
Kisha wale watumishi wa mashua wakasemezana: Tupige kura tupate kujua hasara hii imetupata kwa ajili ya kosa la nani. Basi, wakapiga kura; kura ikamwangukia Yona.
8
Kwa hiyo wakaanza kumwuliza: Sasa utuambie! Kwa nini hasara hii inatupata? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Inchi yako ni gani? Uko wa kabila gani?
9
Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.
10
Kisha Yona akawaelezea kwamba alikuwa anamukimbia Yawe. Kusikia hayo, watu hao wakazidi kuogopa, wakamwambia: Kwa sababu gani umefanya vile?
11
Wakati huo wote, bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Basi, wakamwuliza Yona: Tukufanye nini kusudi bahari itulie?
12
Yona akawajibu: Munikamate na kunitupa katika bahari, nayo bahari itatulia, maana ninaona wazi kwamba zoruba hii imewapata kwa sababu yangu mimi.
13
Watumishi wale wakajaribu kuvuta makasia wapate kuifikisha mashua yao inchi kavu, lakini hawakufanikiwa kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia.
14
Basi, wakamulilia Yawe wakisema: Ee Yawe, tunakusihi usituangamize kwa kuutoa uzima wa mutu huyu, wala usituazibu kwa kumwanga damu ya mutu asiyekuwa na kosa. Wewe, ee Yawe, umefanya unavyopenda.
15
Basi, wakamukamata Yona, wakamutupa ndani ya bahari na palepale bahari ikatulia.
16
Watu hao wakamwogopa sana Yawe, wakamutolea sadaka na kufanya viapo.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4