bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jonah 3
Jonah 3
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 4 →
1
Neno la Yawe lilimufikia Yona mara ya pili kusema hivi:
2
Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uwatangazie watu ujumbe ninaokupa.
3
Basi, Yona akaondoka, akaenda Ninawe kama vile Yawe alivyomwagiza. Muji wa Ninawe ulikuwa mukubwa sana. Upana wake ulikuwa mwendo wa siku tatu.
4
Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!
5
Basi, watu wa Ninawe wakauamini ujumbe wa Mungu, wakatangaza kufunga kula chakula, na kwamba kila mumoja wao, mukubwa kama vile mudogo, avae gunia.
6
Habari hizi zikamufikia mufalme wa Ninawe, naye akaondoka juu ya kiti chake cha kifalme, akavua nguo yake ya kifalme, akavaa gunia na kuikaa katika majivu.
7
Kisha mufalme akawatangazia wakaaji wa Ninawe: Mimi mufalme, pamoja na wakubwa wangu, ninatoa amri hii: Kusikuwe mutu yeyote, ngombe au nyama yeyote wa kufugwa, atakayeonja kitu chochote. Hairuhusiwi kwa mutu yeyote au nyama kula au kunywa.
8
Watu wote na nyama wavae gunia. Kila mutu amwombe Mungu na kumusihi kwa moyo. Kila mumoja aache uovu wake, aache kutenda kwa ukali.
9
Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!
10
Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4