bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Joshua 12
Joshua 12
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 13 →
1
Hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kunyanganya inchi yao yote iliyokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani kutokea bonde la muto Arnoni mpaka kwenye mulima Hermoni na inchi yote ya Araba upande wa mashariki:
2
Mufalme Sihoni wa Waamori aliyeishi kule Hesiboni na kutawala kutokea kwenye makao yake makubwa kule Aroeri, muji uliokuwa kandokando ya bonde la Arnoni. Alitawala vilevile kuanzia katikati ya bonde mpaka kwenye muto Yaboki ambao ulikuwa mupaka wa inchi ya Waamoni, ni kusema nusu ya inchi ya Gileadi.
3
Vilevile, alitawala inchi yote ya Araba, kutokea bahari ya Kineroti, upande wa mashariki, mpaka Beti-Yesimoti kwenye bahari ya Chumvi na kuendelea mpaka chini ya mulima Pisiga.
4
Mwingine ni mufalme Ogi mumoja wa Warefaimu waliobaki, ambaye alitawala Basani na alikaa Asitaroti au Edirei.
5
Utawala wake ulienea mpaka kule kwenye mulima Hermoni, kule Saleka, Basani yote mpaka kwa mipaka ya Wagesuri na Wamakati, nusu ya Gileadi hata kwa mupaka wa inchi ya mufalme Sihoni wa Hesiboni.
6
Musa mutumishi wa Yawe pamoja na Waisraeli aliwashinda wafalme hao, akawapatia inchi hizo makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase zikuwe mali yao kabisa.
7
Kisha Yoshua pamoja na Waisraeli waliwashinda wafalme wote wa eneo lote linalokuwa upande wa magaribi wa muto Yordani, kuanzia Bali-Gadi katika bonde la Lebanoni mpaka kwenye mulima uliokuwa mutupu wa Halaki upande wa kusini karibu na Seiri. Yoshua akayagawanyia makabila ya Israeli inchi hizo zikuwe mali yao kabisa.
8
Inchi hizo zilikuwa pamoja na maeneo ya milima, inchi ya bonde, eneo la Araba, miteremuko ya milima, maeneo ya jangwa, na eneo la Negebu; inchi zilizokuwa za Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
9
Wafalme walioshindwa walikuwa, mumoja kwa mwengine: mufalme wa Yeriko, mufalme wa Ai muji unaokuwa karibu na Beteli,
10
mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni,
11
mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi,
12
mufalme wa Eguloni, mufalme wa Gezeri,
13
mufalme wa Debiri, mufalme wa Gederi,
14
mufalme wa Horma, mufalme wa Aradi,
15
mufalme wa Libuna, mufalme wa Adulamu,
16
mufalme wa Makeda, mufalme wa Beteli,
17
mufalme wa Tapua, mufalme wa Heferi,
18
mufalme wa Afeki, mufalme wa Lasaroni,
19
mufalme wa Madoni, mufalme wa Hazori,
20
mufalme wa Simuroni-Meroni, mufalme wa Akisafu,
21
mufalme wa Tanaki, mufalme wa Megido,
22
mufalme wa Kedesi, mufalme wa Yokinamu muji unaokuwa kwenye mulima Karmeli,
23
mufalme wa Dori katika sehemu ya Nafoti-Dori, mufalme wa Goyimu kule Gilgali na
24
mufalme wa Tirza. Jumla ya wafalme hao ni makumi tatu na mumoja.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24