bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Judges 10
Judges 10
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 11 →
1
Nyuma ya kifo cha Abimeleki, Tola mwana wa Puha mujukuu wa Dodo, wa kabila la Isakari, akatokea kuwakomboa Waisraeli. Tola aliishi Samiri katika inchi ya milima ya Efuraimu.
2
Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka makumi mbili na mitatu, kisha akakufa na kuzikwa kule Samiri.
3
Nyuma ya Tola, kukatokea Yairi wa Gileadi, akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka makumi mbili na mbili.
4
Yairi alikuwa na watoto wa kiume makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi tatu na walikuwa na miji makumi tatu katika inchi ya Gileadi, ambayo mpaka leo inaitwa Miji ya Yairi.
5
Yairi akakufa na kuzikwa kule Kamoni.
6
Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.
7
Hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli, naye akawatia katika mikono ya Wafilistini na Waamoni.
8
Kwa miaka kumi na minane hao waliwatesa na kuwagandamiza Waisraeli walioishi kule Gileadi katika eneo la Waamori upande wa mashariki wa muto Yordani.
9
Waamoni nao walivuka muto Yordani kupigana na makabila ya Yuda, Benjamina na Efuraimu. Nao Waisraeli wakapata taabu sana.
10
Basi wakamulilia Yawe, wakisema: “Tumetenda zambi mbele yako, maana tumekuacha wewe Mungu wetu, tukatumikia Mabali.”
11
Naye Yawe akawaambia: “Mimi sikuwakomboa kutoka kwa Wamisri, Waamoni, Waamori, na Wafilistini?
12
Wasidoni, Waamaleki na Wamidiani waliwagandamiza nanyi mukanililia, nami nikawakomboa toka katika mikono yao.
13
Hata hivyo ninyi mumeniacha, mukatumikia miungu mingine. Kwa hiyo sitawakomboa tena.
14
Muende muililie hiyo miungu muliyoichagua. Muache hiyo iwakomboe katika taabu zenu!”
15
Lakini Waisraeli wakamwambia Yawe: “Tumetenda zambi. Utufanye vile unavyopenda, lakini tunakuomba utuokoe leo.”
16
Kisha wakaitupilia mbali miungu ya kigeni, wakamutumikia tena Yawe. Yawe hakuweza kuvumilia zaidi kuona taabu za Waisraeli.
17
Waamoni wakajikusanya wakapiga kambi yao kule Gileadi. Waisraeli nao wakakusanyika na kupiga kambi yao kule Misipa.
18
Waisraeli na viongozi wao wakaulizana: “Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Atakayefanya hivyo ndiye atakayekuwa kiongozi wa wakaaji wote wa Gileadi.”
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 11 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21