bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Judges 12
Judges 12
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 13 →
1
Watu wa kabila la Efuraimu wakakusanyika, wakavuka muto Yordani wakafika kule Safoni. Kisha wakamwambia Yefuta: “Kwa nini haukutuita tuende pamoja nawe kupigana na Waamoni? Sasa tutaichoma nyumba yako nawe mwenyewe ndani yake.”
2
Yefuta akawaambia: “Mimi pamoja na watu wangu tulikuwa na uadui mukubwa na Waamoni. Niliwaomba munisaidie lakini hamukukuja kuniokoa.
3
Nilipoona kwamba hamukukuja kuniokoa, nikahatarisha maisha yangu, nikavuka kwenda kupigana na Waamoni, naye Yawe akawatia katika mikono yangu. Kwa nini sasa munakuja kupigana na mimi?”
4
Basi, Yefuta akakusanya watu wote wa Gileadi, akapigana na watu wa Efuraimu. Watu wa Gileadi wakawashinda watu wa Efuraimu. Hawa Waefuraimu ndio hao waliokuwa wamesema: “Ninyi watu wa Gileadi ni wakimbizi wa kabila la Efuraimu muliotoka katika kabila la Efuraimu mukaenda kwa kabila la Manase.”
5
Kisha watu wakavishika vivuko vya muto Yordani kwa kuiziba njia ya watu wa Efuraimu. Kila mara mukimbizi alipotokea akiomba kupita kule, watu wa Gileadi walimwuliza: “Wewe ni Mwefuraimu?” Na kama akijibu “Hapana”,
6
walimwambia: “Basi useme neno ‘Shiboleti’ ”. Lakini yeye akisema “Siboleti” kwa sababu hakuweza kulitamka sawasawa, walimukamata na kumwua kule kwenye vivuko vya muto Yordani. Watu elfu makumi ine na mbili wa Efuraimu wakapoteza maisha yao wakati ule.
7
Yefuta alikuwa mwamuzi katika Israeli kwa miaka sita. Kisha akakufa, akazikwa kule Gileadi katika muji wake.
8
Nyuma ya Yefuta, Ibusani wa muji wa Betelehemu akakuwa mwamuzi wa Israeli.
9
Yeye alikuwa na wana makumi tatu na wabinti makumi tatu. Nao wabinti zake aliwaoesha inje ya ukoo wake, na wana aliwaoea wabinti makumi tatu kutoka inje ya ukoo wake. Ibusani alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka saba.
10
Akakufa, akazikwa katika muji wa Betelehemu.
11
Nyuma ya Ibusani, Eloni wa kabila la Zebuluni, akakuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka kumi.
12
Naye akakufa, akazikwa katika muji wa Ayaloni katika inchi ya kabila la Zebuluni.
13
Nyuma ya Eloni, Abudoni mwana wa Hileli wa muji wa Piratoni akakuwa mwamuzi wa Israeli.
14
Yeye alikuwa na watoto wanaume makumi ine na wajukuu makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi saba. Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka minane.
15
Kisha Abudoni akakufa, akazikwa katika muji wa Piratoni katika inchi ya kabila la Efuraimu kwenye eneo la milima ya Waamaleki.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21