bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
/
Job 19
Job 19
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
← Chapter 18
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 20 →
1
Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2
Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno?
3
Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
4
Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
5
Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu;
6
Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake.
7
Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
8
Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.
9
Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
10
Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling'oa kama mti.
11
Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
12
Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
13
Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
14
Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
15
Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao.
16
Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu.
17
Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu.
18
Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena.
19
Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.
20
Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
21
Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.
22
Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu?
23
Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
24
Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
25
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
26
Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
27
Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine.
28
Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
29
Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.
← Chapter 18
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 20 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42