bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
/
Job 21
Job 21
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 22 →
1
Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2
Yasikizeni sana maneno yangu; Jambo hili na liwe faraja yenu.
3
Niacheni, nami pia nitanena; Tena nikiisha nena, zidini kudhihaki.
4
Mimi, je! Mashitaka yangu yamhusu mwanadamu? Nami kwa nini nisikose kusubiri?
5
Niangalieni, mkastaajabu, Mkaweke mkono kinywani.
6
Hata nikumbukapo nahuzunika, Na utisho wanishika mwilini mwangu.
7
Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?
8
Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao.
9
Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi.
10
Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng'ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.
11
Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza.
12
Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi.
13
Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula.
14
Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako.
15
Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
16
Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
17
Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa? Na msiba wao kuwajilia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?
18
Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba?
19
Mwasema, Mungu huwawekea watoto wa mtu huo uovu wake. Na amlipe mwenyewe, ili apate kuujua.
20
Macho yake mwenyewe na yaone uharibifu wake, Akanywe ghadhabu zake Mwenyezi.
21
Kwani ana furaha gani katika mbari yake baada yake, Hesabu ya miezi yake itakapokwisha katwa katikati?
22
Je! Mtu awaye yote atamfundisha Mungu maarifa? Naye ndiye awahukumuye walioko juu.
23
Mmoja hufa katika nguvu zake kamili, Mwenye kukaa salama na kustarehe;
24
Vyombo vyake vimejaa maziwa, Na mafuta ya mifupani mwake ni laini.
25
Mwingine hufa katika uchungu wa roho, Asionje mema kamwe.
26
Wao hulala mavumbini sawasawa, Mabuu huwafunika.
27
Tazama, nayajua mawazo yenu, Na mashauri mnayoazimia kwa uovu juu yangu.
28
Kwa kuwa mwasema, Nyumba ya huyo mkuu i wapi? Na hema waliyoikaa hao waovu i wapi?
29
Je! Hamkuwauliza wapitao njiani? Na maonyo yao hamyajui?
30
Kwamba mwovu huachiliwa katika siku ya msiba? Na kuongozwa nje katika siku ya ghadhabu?
31
Ni nani atakayetangaza njia yake usoni pake? Tena ni nani atakayemlipa kwa hayo aliyofanya?
32
Pamoja na hayo atachukuliwa kaburini, Nao watalinda zamu juu ya ziara lake.
33
Udongo wa bondeni utakuwa tamu kwake, Na watu wote watafuata nyuma yake, Kama vile walivyomtangulia watu wasiohesabika.
34
Basi imekuwaje ninyi kunituza moyo bure, Kwa kuwa katika jawabu zenu unasalia uongo tu.
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 22 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42