bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
/
Proverbs 4
Proverbs 4
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 5 →
1
Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.
2
Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri; Msiiache sheria yangu.
3
Maana nalikuwa mwana kwa baba yangu, Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu.
4
Naye akanifundisha, akaniambia, Moyo wako uyahifadhi maneno yangu; Shika amri zangu ukaishi.
5
Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau; Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu.
6
Usimwache, naye atakuhifadhi; Umpende, naye atakulinda.
7
Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
8
Umtukuze, naye atakukuza; Atakupatia heshima, ukimkumbatia.
9
Atakupa neema kuwa kilemba kichwani; Na kukukirimia taji ya uzuri.
10
Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu; Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
11
Nimekufundisha katika njia ya hekima; Nimekuongoza katika mapito ya unyofu.
12
Uendapo, hatua zako hazitadhiikika, Wala ukipiga mbio hutajikwaa.
13
Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.
14
Usiingie katika njia ya waovu, Wala usitembee katika njia ya wabaya.
15
Jiepushe nayo, usipite karibu nayo, Igeukie mbali, ukaende zako.
16
Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara; Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.
17
Maana wao hula mkate wa uovu, Nao hunywa divai ya jeuri.
18
Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi kung'aa hata mchana mkamilifu.
19
Njia ya waovu ni kama giza; Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho.
20
Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu.
21
Zisiondoke machoni pako; Uzihifadhi ndani ya moyo wako.
22
Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote.
23
Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24
Kinywa cha ukaidi ukitenge nawe, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.
25
Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.
26
Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike;
27
Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni.
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 5 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31