bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
/
Proverbs 7
Proverbs 7
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 8 →
1
Mwanangu, yashike maneno yangu, Na kuziweka amri zangu akiba kwako.
2
Uzishike amri zangu ukaishi, Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.
3
Zifunge katika vidole vyako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4
Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu; Mwite ufahamu jamaa yako mwanamke.
5
Wapate kukulinda na malaya, Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.
6
Maana katika dirisha la nyumba yangu Nalichungulia katika shubaka yake;
7
Nikaona katikati ya wajinga, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili,
8
Akipita njiani karibu na pembe yake, Akiishika njia iendayo nyumbani kwake,
9
Wakati wa magharibi, wakati wa jioni, Usiku wa manane, gizani.
10
Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
11
Ana kelele, na ukaidi; Miguu yake haikai nyumbani mwake.
12
Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia.
13
Basi akamshika, akambusu, Akamwambia kwa uso usio na haya,
14
Kwangu ziko sadaka za amani; Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;
15
Ndiyo maana nikatoka nikulaki, Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona.
16
Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri, Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.
17
Nimetia kitanda changu manukato, Manemane na udi na mdalasini.
18
Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.
19
Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;
20
Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.
21
Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.
22
Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng'ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;
23
Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.
24
Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.
25
Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake.
26
Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.
27
Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 8 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31