bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
/
Proverbs 12
Proverbs 12
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 13 →
1
Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
2
Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
3
Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu; Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
4
Mwanamke mwema ni taji ya mumewe; Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5
Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6
Maneno ya waovu huotea damu; Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7
Waovu huangamia, hata hawako tena; Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8
Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake; Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9
Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa, Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10
Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11
Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12
Asiye haki hutamani nyavu za wabaya; Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13
Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14
Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake; Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
15
Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16
Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
17
Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
18
Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19
Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
20
Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21
Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote; Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22
Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23
Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
24
Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.
25
Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha; Bali neno jema huufurahisha.
26
Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake; Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
27
Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.
28
Katika njia ya haki kuna uhai; Wala hakuna mauti katika mapito yake.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31