bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
/
Proverbs 15
Proverbs 15
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 16 →
1
Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
2
Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
3
Macho ya BWANA yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.
4
Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5
Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
6
Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
7
Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
8
Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
9
Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
10
Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11
Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12
Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13
Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14
Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa; Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15
Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya; Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16
Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17
Chakula cha mboga penye mapendano; Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
18
Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
19
Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20
Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21
Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22
Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
23
Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24
Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.
25
BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26
Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maneno yapendezayo ni safi.
27
Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.
28
Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
29
BWANA yu mbali na wasio haki; Bali huisikia sala ya mwenye haki.
30
Mng’ao wa macho huufurahisha moyo; Habari njema huinenepesha mifupa.
31
Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.
32
Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.
33
Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 16 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31