bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Samuel 4
2 Samuel 4
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 5 →
1
Isiboseti mwana wa Saulo, aliposikia kwamba Abeneri ameuawa kule Hebroni, alivunjika moyo na watu wote wa Israeli walifazaika.
2
Mwana huyo wa Saulo alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa makundi yake ya waaskari. Mumoja aliitwa Bana na mwingine Rekabu. Hao walikuwa wana wa Rimoni, mutu wa kabila la Benjamina wa muji wa Beroti (kwa maana Beroti vilevile ulikuwa mali ya kabila la Benjamina).
3
Wakaaji wa Beroti walikimbilia Gitaimu, na wameishi kule kama wageni mpaka leo.
4
Yonatani mwana wa Saulo alikuwa na mutoto aliyekuwa kilema wa miguu. Mutoto huyo aliitwa Mefiboseti. Mefiboseti alikuwa na umri wa miaka mitano wakati habari za kifo cha Saulo na Yonatani ziliposikilika kutoka Yezereheli. Kwa wakati ule, mulezi wake aliposikia kwamba Saulo na Yonatani waliuawa kule Yezereheli, akamukamata Mefiboseti na kukimbia naye. Lakini alipokuwa anakimbia kwa haraka, mutoto huyo alianguka na kuwa kilema.
5
Rekabu na Bana wana wa Rimoni wa Beroti wakaenda kwa nyumba ya Isiboseti. Walifika kule wakati wa jua kali ya muchana, Isiboseti alipokuwa anapumzika mwake.
6
Waliingia ndani ya nyumba wakijifanya sawa vile wanataka kukamata ngano, walimukuta Isiboseti amelala juu ya kitanda chake ndani ya chumba chake cha kulala, wakamuchoma mukuki katika tumbo. Kisha kumwua hivyo hao wandugu wawili walimukata kichwa wakatoroka wakikibeba. Walipitia njia ya Araba, wakasafiri usiku kucha.
8
Halafu walikamata kichwa cha Isiboseti na kumupelekea Daudi kule Hebroni. Nao wakamwambia mufalme Daudi: “Hiki ni kichwa cha Isiboseti mwana wa Saulo ambaye ni adui yako aliyekuwa anataka kuyaangamiza maisha yako. Yawe leo amekulipizia kisasi juu ya Saulo na wazao wake.”
9
Lakini Daudi akamujibu Rekabu na ndugu yake Bana, wana wa Rimoni wa Beroti: “Kama vile Yawe anavyoishi, yeye ameyakomboa maisha yangu kutoka kila adui.
10
Yule mutu aliyekuja kuniambia kwamba Saulo amekufa, akizani kwamba ananiletea habari njema, nilimukamata na kumwua kule. Hivyo ikakuwa ndiyo zawadi niliyomupa kutokana na habari yake.
11
Mutu mwovu anapomwua mutu wa haki akiwa katika kitanda ndani ya nyumba yake, basi si ni jambo la haki kwangu kumulipiza kwa sababu ya kumwanga damu kwa kumwondosha toka katika dunia?”
12
Daudi akawaamuru vijana wake, nao wakawaua. Wakawakata mikono na miguu. Halafu wakawatundika juu ya muti pembeni ya kisima kule Hebroni. Lakini walikichukua kichwa cha Isiboseti na kukizika katika kaburi la Abeneri kule Hebroni.
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 5 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24