bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Samuel 5
2 Samuel 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 6 →
1
Kisha makabila yote ya Waisraeli yalimwendea Daudi kule Hebroni, na kumwambia: “Angalia, sisi ni mwili na damu yako.
2
Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”
3
Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.
4
Daudi alikuwa na umri wa miaka makumi tatu alipoanza kutawala, na alitawala kwa muda wa miaka makumi ine.
5
Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.
6
Kisha mufalme na watu wake walikwenda Yerusalema kuwashambulia Wayebusi waliokuwa wenyeji wa inchi hiyo. Lakini wao wakamwambia: “Hautaingia ndani ya muji huu, maana vipofu na vilema watakufukuza.” Walimwambia hivyo maana walifikiri kwamba Daudi asingeweza kuingia katika muji ule.
7
Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.
8
Siku hiyo, Daudi alisema: “Mutu yeyote atakayewapiga Wayebusi apitie kwenye mufereji wa maji kwa kuwashambulia vilema na vipofu ambao roho yangu inawachukia.” Ndiyo maana watu wanasema: “Vipofu na vilema hawataingia katika nyumba.”
9
Daudi alikaa kwenye kikingio hicho. Akakiita: “Muji wa Daudi.” Daudi akaongeza muji, akianzia uwanja wa Milo kuelekea ndani.
10
Naye Daudi akazidi kuwa na uwezo zaidi kwa sababu Yawe, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.
11
Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.
12
Hivyo, Daudi akatambua kwamba Yawe amemwimarisha akuwe mufalme wa Israeli, na kwamba ameutukuza ufalme wake kwa ajili ya watu wake Waisraeli.
13
Daudi alijitwalia wahabara na kuoa wake zaidi wa kule katika muji wa Yerusalema kisha kutoka Hebroni. Hao, wakamuzalia wana na wabinti.
14
Haya ndiyo majina ya wana ambao wake zake walimuzalia kule Yerusalema: Samua, Sobabu, Natani, Solomono,
15
Ibuhari, Elisua, Nefegi, Yafia,
16
Elisama, Eliada na Elifeleti.
17
Wafilistini waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mufalme wa Waisraeli, wote walitoka kwenda kumutafuta, lakini yeye alipata habari, akaingia ndani ya makimbilio.
18
Wafilistini walifika na kujitawanya kwenye Bonde la Refaimu.
19
Basi, Daudi alimwuliza Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia Daudi: “Kwenda, maana hakika nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”
20
Basi, Daudi akafika Bali-Perasimu na kuwashinda Wafilistini. Halafu akasema: “Yawe amepita katikati ya waadui zangu kama mafuriko ya maji yanayoenda mbio.” Kwa hiyo pahali pale pakaitwa “Bwana Anayepita Katikati”.
21
Wafilistini waliziacha sanamu zao za miungu pahali pale, naye Daudi na watu wake wakazikamata.
22
Kwa mara ya pili, Wafilistini walifika tena na kujitawanya kwenye bonde la Refaimu.
23
Daudi alipomwomba Yawe shauri, Yawe alimwambia: “Usiwashambulie kutoka hapa unapokuwa, lakini zunguka nyuma yao na kuwashambulia kutokea mbele ya miti ya miforosadi.
24
Na mara moja mutakaposikia vishindo vya miguu kwenye vilele vya miforosadi hiyo, halafu ujipe moyo maana nitakuwa nimetoka kwa kukutangulia kuwapiga waaskari wa Wafilistini.”
25
Daudi alifanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe, naye akawapiga Wafilistini kutokea Geba mpaka Gezeri.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 6 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24