bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Leviticus 22
Leviticus 22
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 23 →
1
Yawe akamwambia Musa:
2
Umwambie Haruni na wana wake makuhani waheshimu vitu ambavyo Waisraeli wametakasa kwa ajili yangu, kusudi wasichafue jina langu takatifu. Mimi ni Yawe.
3
Uwaambie hivi: Kama mumoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote akikaribia vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wamevitakasa kwa ajili yangu mimi Yawe akiwa muchafu, mutu huyu atatengwa nami. Mimi ni Yawe.
4
Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,
5
au akigusa kiumbe chochote chenye kutambaa ambacho kinamufanya mutu kuwa muchafu au mutu ambaye anaweza kumuchafua wa aina yoyote,
6
mutu huyu, atakuwa muchafu mpaka magaribi na haruhusiwi kula vyakula vitakatifu mpaka pale atakapokuwa ameoga.
7
Jua litakapotua ndipo atakapokuwa safi. Nyuma ya pale ataweza kula vyakula vitakatifu maana hicho ndicho chakula chake.
8
Kuhani asikule nyama yoyote ya nyama aliyekufa peke yake au kuuawa na nyama wa pori, kusudi asijichafue. Mimi ni Yawe.
9
Kwa hiyo, makuhani washike agizo langu, kusudi wasifanye zambi na kuuawa. Mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.
10
Mutu asiyekuwa wa ukoo wa makuhani haruhusiwi kula chakula kitakatifu. Hata mugeni wa kuhani au mutumishi wake haruhusiwi kula.
11
Lakini kama kuhani amenunua mutumwa kwa kuwa mali yake, basi, yule mutumwa anaruhusiwa kula na vilevile wale waliozaliwa katika nyumba yake.
12
Kama binti ya kuhani ameolewa na mutu asiyekuwa kuhani, haruhusiwi kula sadaka ya vitu vitakatifu.
13
Lakini kama binti ya kuhani ni mujane au amefukuzwa na mume wake na hana mutoto, naye amerudi kwa baba yake na kukaa naye kama vile alipokuwa kijana, basi, anaweza kula chakula cha baba yake. Hata hivyo, mugeni haruhusiwi kula chakula hicho.
14
Kama mutu mwingine akikula chakula kitakatifu bila kujua, basi, atalipa nyongezo ya sehemu moja ya tano pamoja na kipimo sawasawa alichokula na kumurudishia kuhani.
15
Kuhani asichafue vitu ambavyo Waisraeli wamemutolea Yawe
16
na hivyo kufanya watu wabebe sababu ya uovu na makosa yao kwa kula vitu vyao vitakatifu. Mimi Yawe ndiye ninayetakasa vitu hivyo.
17
Yawe akamwambia Musa:
18
Umwambie Haruni na wana wake makuhani na Waisraeli wote hivi: Kama mutu yeyote kati yenu au mugeni yeyote anayeishi katika Israeli akitoa sadaka yake, ikuwe ni ya kutimiza kiapo au sadaka ya mapenzi ya kumutolea Yawe kwa kuteketezwa,
19
kusudi apate kukubalika, atatoa katika ngombe dume au katika kondoo beberu asiyekuwa na kilema.
20
Inakatazwa kutoa chochote kinachokuwa na kilema maana hakitakubaliwa kwa faida yenu.
21
Mutu yeyote anapomutolea Yawe sadaka ya amani kwa kutimiza kiapo au sadaka ya mapenzi kutoka katika kundi lake la mifugo, kusudi akubaliwe anapaswa kuwa nyama mukamilifu, nyama huyo asikuwe na kilema chochote.
22
Usimutolee Yawe nyama yeyote anayekuwa kipofu, kilema, aliyevunjika, anayetokwa na usaha, mwenye upele au ukurutu, wala usiwatoe kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu ya Yawe.
23
Ngombe dume au mwana-kondoo anayekuwa na kiungo kimoja kirefu au kifupi kuliko kawaida wanaweza kumutoa sadaka ya mapenzi. Lakini huyo usimutoe kuwa sadaka ya kutimiza kiapo.
24
Nyama ambaye kiungo chake cha uzazi kimeumizwa, kimepondwa, kimevunjwa au kimekatwa, usimutolee Yawe wala kumutoa kama vile sadaka katika inchi yako.
25
Wala usipokee kutoka kwa wageni nyama wa namna hiyo na kunitolea mimi Mungu wako kama chakula. Nyama hao wana kilema kwa vile wamekatwa na hawatakubaliwa kwa faida yenu.
26
Yawe akamwambia Musa:
27
Ngombe dume, kondoo dume au beberu akizaliwa atabaki na mama yake kwa siku saba. Lakini tangu siku ya nane anaweza kutolewa kwa Yawe kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto.
28
Lakini usichinje ngombe au kondoo siku moja pamoja na kitoto chake.
29
Utakaponitolea mimi Yawe sadaka ya shukrani utaitoa kwa namna ambayo itakufanya ukubaliwe.
30
Nyama huyo ni lazima akuliwe siku hiyohiyo. Musiache kitu mpaka kesho yake asubui. Mimi ni Yawe.
31
Kwa hiyo mutashika na kutimiza amri zangu. Mimi ni Yawe.
32
Musichafue jina langu takatifu, maana ni lazima niheshimiwe kati ya watu wa Israeli. Mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.
33
Ni mimi niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu. Mimi ni Yawe.
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 23 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27