bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Leviticus 24
Leviticus 24
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 25 →
1
Yawe akamwambia Musa:
2
Uwaamuru watu wa Israeli wakuletee mafuta safi kwa ajili ya taa kusudi taa hiyo iendelee kuwaka siku zote.
3
Haruni ataweka taa hiyo ndani ya hema la mukutano, inje ya pazia la Sanduku la Agano kusudi ipate kuwaka mbele yangu tangu usiku mpaka asubui. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu.
4
Ataweka hizo taa katika kinara cha taa cha zahabu safi ziwake siku zote mbele ya Yawe.
5
Twaa unga laini, kilo kumi na mbili na kupika mikate kumi na miwili.
6
Mikate hiyo itapangwa kwa mistari miwili juu ya meza ya zahabu safi, kila mustari mikate sita.
7
Kila mustari utautia ubani safi kusudi uambatane na mikate hiyo na kuwa sehemu ya sadaka ya kuteketezwa ya ukumbusho kwa Yawe.
8
Kila siku ya Sabato Haruni ataipanga sawasawa katika mustari mbele yangu mimi Yawe kwa ajili ya watu wa Israeli kama vile agano la milele.
9
Haruni na wazao wake peke yao ndio wanaoruhusiwa kula mikate hiyo maana ni mitakatifu kabisa kwa sababu ni sehemu ya sadaka ninazotolewa mimi Yawe kwa moto. Hiyo ni haki yao milele.
10
Siku moja kukatokea fujo kule katika kambi kati ya Mwisraeli mumoja na kijana mumoja wa mama Mwisraeli lakini baba Mumisri.
11
Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa,
12
wakamutia katika kifungo mpaka pale watakapofunuliwa mapenzi ya Yawe.
13
Basi, Yawe akamwambia Musa:
14
Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.
15
Nawe uwaambie Waisraeli kwamba mutu yeyote atakayemulaani Mungu wake atabeba lazima ya zambi yake.
16
Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.
17
Mutu yeyote anayeua mutu mwingine anapaswa naye kuuawa.
18
Mutu yeyote anayeua nyama wa mwenzake anapaswa kutoa malipo: uzima kwa uzima.
19
Mutu yeyote anayemwumiza mwenzake, anapaswa naye aumizwe sawasawa na vile alivyomwumiza mwenzake,
20
akimuvunja mufupa naye atavunjwa mufupa, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kila mutu anayemwumiza mwenzake anapaswa naye aumizwe kulingana na tendo lake.
21
Anayemwua nyama anapaswa kutoa malipo, lakini mutu yeyote akimwua mutu mwingine anapaswa naye auawe.
22
Sheria hii inaelekea mugeni na mwenyeji. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
23
Basi, Musa akawaambia Waisraeli hayo yote. Wakamupeleka yule mutu aliyelaani Yawe inje ya kambi, wakamwua kwa kumupiga mawe. Ndivyo Waisraeli walivyofanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 25 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27