bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Matthew 16
Matthew 16
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 17 →
1
Wafarisayo na Wasadukayo wakamufikia Yesu. Nao wakamupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake unatoka kwa Mungu.
2
Lakini akawajibu: “Kwa wakati wa magaribi munapoona kwamba mawingu ni meupe, munasema kwamba hali ya hewa itakuwa nzuri kesho yake.
3
Na asubui munapoona kwamba mawingu ni meusi munasema kwamba mvua itanyesha. Munajua kutambua hali ya mawingu, lakini hamuwezi kujua vitambulisho vya nyakati hizi.
4
Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataonyeshwa kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.” Kisha Yesu akawaacha na kujiendea.
5
Wakati wanafunzi walipovuka ziwa kwenda ngambo ingine, walikuwa wamesahau kupeleka mikate.
6
Yesu akawaambia: “Muangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”
7
Wanafunzi wakaanza kusemezana hivi wao kwa wao: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”
8
Yesu akatambua maneno waliyosema, basi akawauliza: “Ee ninyi wenye imani ndogo, sababu gani munasemezana kati yenu juu ya kukosa mikate?
9
Hamujaelewa bado? Hamukumbuki ile mikate mitano niliyoshibisha nayo watu elfu tano, nayo ile hesabu ya vitunga mulivyojaza?
10
Hamukumbuki vilevile ile mikate saba niliyoshibisha nayo watu elfu ine, na ile hesabu ya vitunga mulivyojaza?
11
Namna gani hamwelewi kwamba sisemi nanyi juu ya mikate, nilipowaambia kwamba mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”
12
Halafu wanafunzi wakafahamu kwamba Yesu hakuwaambia kwamba wafanye angalisho na chachu ya mikate, lakini na mafundisho ya Wafarisayo na Wasadukayo.
13
Yesu alipofika pande za muji Kaisaria Filipi, akawauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema kwamba Mwana wa Mutu ni nani?”
14
Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba yeye ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba yeye ni Elia, na wengine wanasema ni Yeremia au mumoja wa manabii wengine.”
15
Halafu Yesu akawauliza: “Na ninyi munasema kwamba mimi ni nani?”
16
Simoni Petro akamujibu: “Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu Mwenye Uzima.”
17
Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.
18
Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.
19
Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni; chochote utakachokikataza katika dunia, kitakatazwa mbinguni vilevile, na chochote utakachokiruhusu katika dunia, kitaruhusiwa mbinguni vilevile.”
20
Kisha Yesu akawakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mutu kwamba yeye ndiye Kristo.
21
Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.
22
Basi Petro akamwita Yesu pembeni na kuanza kumukaripia, akisema: “Ee Bwana, isikuwe vile! Mambo yale hayatakufikia hata kidogo!”
23
Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”
24
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.
25
Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake, ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu, ataupata tena.
26
Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.
27
Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.
28
Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajamwona Mwana wa Mutu akikuja katika Ufalme wake.”
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 17 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28