bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Matthew 26
Matthew 26
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 27 →
1
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo yote, akawaambia wanafunzi wake:
2
“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”
3
Wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu wakakusanyika ndani ya nyumba ya Kuhani Mukubwa, aliyeitwa Kayafa,
4
nao wakafanya shauri la kumukamata Yesu kwa werevu na kumwua.
5
Lakini walijisemesha: “Tusimukamate kwa wakati wa karamu, kusudi fujo isitokee kati ya watu.”
6
Yesu alipokuwa Betania katika nyumba ya mutu aliyeitwa Simoni Mukoma,
7
mwanamuke mumoja aliingia ndani ya nyumba, akiwa na chupa la jiwe lenye kuwa na marasi ya bei kali, akaimimia juu ya kichwa cha Yesu walipokuwa wakikula.
8
Wanafunzi wake walipoona jambo lile, wakachukizwa na kusema: “Kwa nini kupoteza mali namna hii?
9
Marasi hii ingeuzishwa kwa bei kali na kuwagawanyia wamasikini mali ile!”
10
Lakini Yesu akatambua mawazo yao na kuwaambia: “Sababu gani munamusumbua mwanamuke huyu? Amenitendea jambo zuri.
11
Kwa maana mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, lakini mimi sitakuwa pamoja nanyi siku zote.
12
Mwanamuke huyu amemimia marasi hii juu ya mwili wangu kwa kuutayarisha kwa ajili ya maziko.
13
Kweli ninawaambia: kwa ajili ya kukumbuka mwanamuke huyu, tendo lile alilofanya litaelezwa popote Habari Njema hii itakapohubiriwa katika dunia nzima.”
14
Halafu mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, aliyeitwa Yuda Iskariota, akaenda kwa wakubwa wa makuhani
15
na kuwaambia: “Mutanipa nini kama nikimutoa Yesu kwenu?” Basi wakamupa vikoroti makumi tatu vya feza.
16
Tangia wakati ule Yuda akaanza kutafuta wakati unaokuwa muzuri kwa kumutoa.
17
Siku ya kwanza ya karamu ya sikukuu ya Mukate Usiotiwa Chachu, wanafunzi wakamwendea Yesu na kumwuliza: “Ni wapi unapotaka tukutayarishie karamu ya Pasaka?”
18
Yesu akawaambia kwamba waende katika muji kwa mutu mumoja na kumwambia: “Mwalimu anasema: ‘Siku yangu inakaribia. Mimi na wanafunzi wangu tutakula karamu ya Pasaka kwako.’ ”
19
Nao wanafunzi wakafanya sawa Yesu alivyowaagiza, wakatayarisha karamu ya Pasaka.
20
Ilipokuwa magaribi, Yesu akaikaa kula chakula pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21
Nao walipokuwa wakikula, akasema: “Kweli ninawaambia: mumoja kati yenu atanitoa.”
22
Wanafunzi wakahuzunika sana na kuanza kumwuliza mumoja kwa mumoja: “Bwana, ni mimi?”
23
Yesu akajibu: “Yule aliyechovya mukate pamoja nami ndani ya sahani ndiye atanitoa.
24
Mwana wa Mutu atakufa sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake, lakini ole kwa mutu yule atakayemutoa! Ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa!”
25
Halafu Yuda, aliyemutoa, akamwuliza: “Mwalimu, ni mimi?” Naye Yesu akamujibu: “Wewe umesema.”
26
Walipokuwa wakikula, Yesu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae na mukule, huu ni mwili wangu.”
27
Kisha akatwaa kikombe, akakibariki na kuwapa, akisema: “Mukunywe ninyi wote,
28
kwa maana hii ni damu yangu inayomwangika kwa ajili ya wengi kusudi wasamehewe zambi. Nayo damu hii inahakikisha agano la Mungu.
29
Nami ninawaambia kwamba tangia sasa sitakunywa tena divai mpaka siku ile nitakapoikunywa mupya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30
Nao walipokwisha kuimba, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.
31
Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’
32
Lakini nitakapokwisha kufufuka, nitawatangulia Galilaya.”
33
Petro akamujibu: “Hata wote wakianguka, mimi sitaanguka hata kidogo.”
34
Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia kwamba katika usiku huu, mbele jogoo hajawika utakuwa umenikana mara tatu.”
35
Lakini Petro akamwambia: “Hata ikinipasa kufa pamoja nawe, sitakukana hata kidogo.” Na wanafunzi wote wengine wakasema sawasawa naye.
36
Kisha Yesu pamoja na wanafunzi wake wakafika katika bustani inayoitwa Getesemane. Na Yesu akawaambia: “Muikae hapa, kwa wakati ninapokwenda kuomba kule.”
37
Na akatwaa Petro na wana wawili wa Zebedayo na kwenda nao. Akaanza kuhuzunika na kuhangaika.
38
Halafu akawaambia: “Ninahuzunika sana, karibu kufa! Mubakie hapa na mukeshe pamoja nami.”
39
Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”
40
Kisha akarudi pahali pale alipowaacha wale wanafunzi, akawakuta wamelala usingizi. Akamwambia Petro: “Hamukuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja tu?
41
Mukeshe na muombe, kusudi musianguke katika majaribu; kwa maana roho ni hodari, lakini mwili ni zaifu.”
42
Akawaacha tena kwa mara ya pili, akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama kikombe hiki cha mateso hakiwezi kupita mbali nami, bila mimi kukikunywa, basi mapenzi yako yafanyike!”
43
Aliporudi tena, akawakuta wanafunzi wale wamelala usingizi, kwa maana macho yao yalikuwa yamewezwa sana na usingizi.
44
Yesu akawaacha tena, na kwenda kuomba kwa mara ya tatu, akirudilia maombi yale yale.
45
Kisha akarudi kwenye wanafunzi wake na kuwaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Angalia, saa imetimia, sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.
46
Musimame, tuende! Angalia, yule anayenitoa amefika karibu!”
47
Yesu alipokuwa hajamaliza kusema, Yuda, mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, akafika pamoja na kundi kubwa la watu wenye panga na magongo. Hawa wote walikuwa wametumwa na wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu.
48
Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, aliwapa kitambulisho hiki: “Yule nitakayemubusu ndiye yeye, mumukamate.”
49
Yuda alipofika, akamujongelea Yesu, na kumwambia: “Jambo, Mwalimu.” Na kisha akamubusu.
50
Lakini Yesu akamwambia: “Rafiki, ufanye lililokuleta.” Halafu watu wale wakajongea na kumukamata Yesu na kumufunga.
51
Na mumoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akachomoa upanga wake, akamupiga mutumishi wa Kuhani Mukubwa, akamukata sikio.
52
Halafu Yesu akamwambia: “Rudisha upanga wako katika kifuko chake, kwa maana yeyote anayetumia upanga, atauawa kwa upanga.
53
Haujui kwamba ninaweza kumwomba Baba yangu musaada na mara moja angenitumia zaidi ya makundi kumi na mawili ya wamalaika?
54
Lakini namna gani yangetimia Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba mambo haya yanapaswa kuwa hivi?”
55
Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.
56
Mambo haya yote yamefanyika kusudi maneno yanayosemwa na manabii katika Maandiko Matakatifu yapate kutimia.” Basi wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
57
Wale waliomukamata Yesu wakamupeleka kwa Kuhani Mukubwa Kayafa, pahali walimu wa Sheria na wasimamizi wa watu walipokuwa wamekusanyika.
58
Lakini Petro akamufuata Yesu kwa mbali, hata akaingia ndani ya upango wa Kuhani Mukubwa. Akaingia katika kiwanja, akaikaa pamoja na walinzi kusudi aone mambo yatakayotokea.
59
Wakubwa wa makuhani na wakubwa wote wa Baraza Kubwa walitafuta mashitaki ya uongo juu ya Yesu, kusudi wapate kumwua.
60
Lakini hawakupata neno, ijapokuwa watu wengi walikuja kumusingizia maneno ya uongo. Mwisho watu wawili wakafika
61
na kusema: “Mutu huyu alisema kwamba anaweza kubomoa hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa muda wa siku tatu.”
62
Kuhani Mukubwa akasimama na kumwuliza Yesu: “Haujibu hata neno? Watu hawa wanakushitakia nini?”
63
Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
64
Yesu akamujibu: “Wewe umesema. Lakini zaidi ya hiyo, ninawaambia ninyi kwamba mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka karibu na Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”
65
Halafu Kuhani Mukubwa akapasua nguo zake na kusema: “Mutu huyu amemutukana Mungu! Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Angalia, munatoka kusikia jinsi alivyomutukana Mungu.
66
Munawaza nini?” Nao wakajibu: “Anastahili kufa.”
67
Halafu wamoja wakamutemea mate juu ya uso, na kumupiga ngumi. Na wengine wakamupiga makofi,
68
wakisema: “Ewe Kristo, tambua ni nani aliyekupiga!”
69
Wakati ule Petro alikuwa akiikaa inje katika kiwanja. Mutumishi mumoja mwanamuke akamufikia na kumwambia: “Wewe vilevile ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70
Lakini akakana mbele ya wote waliokuwa pale, akisema: “Sijui maneno unayotaka kusema.”
71
Petro alipotoka inje kwa mulango wa upango, mutumishi mwingine mwanamuke akamwona na kuwaambia wale waliokuwa pale: “Huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
72
Lakini Petro akakana tena akaapa akisema: “Ninaapa ya kuwa simujui mutu huyu!”
73
Nyuma kidogo, wale waliosimama pale, wakamufikia Petro na kumwambia: “Hakika wewe ni mumoja wao, kwa maana hata usemi wako unakutambulisha.”
74
Halafu Petro akaanza kusema: “Nilaaniwe ikiwa ninasema uongo! Ninaapa kwamba simujui mutu huyu!” Na mara moja jogoo akawika,
75
naye Petro akakumbuka maneno yale Yesu aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika, atakuwa amemukana mara tatu. Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 27 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28