bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Matthew 5
Matthew 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 6 →
1
Yesu alipoona yale makundi ya watu, alipanda kwenye kilima. Alipokwisha kuikaa, wanafunzi wake wakamujongelea.
2
Naye akaanza kuwafundisha akisema:
3
“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!
4
Heri wale wanaokuwa na huzuni, maana Mungu atawafariji!
5
Heri wale wanaokuwa wapole, maana watarizi dunia!
6
Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!
7
Heri wale wanaokuwa na huruma, maana Mungu atawahurumia!
8
Heri wale wanaokuwa na moyo safi, maana watamwona Mungu!
9
Heri wale wanaoleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu!
10
Heri wale wanaoteswa kwa ajili ya haki, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!
11
“Heri ninyi, wakati watu wanapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya ubaya kwa sababu yangu.
12
Mufurahi na kushangilia, kwa sababu munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi walivyowatesa manabii walioishi mbele yenu.
13
“Ninyi ni kama chumvi kwa watu wote. Lakini kama chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini ipate tena kukolea? Haifai tena hata kidogo, inabakilia kutupwa na kukanyagwa na watu.
14
“Ninyi ni kama mwangaza katika dunia. Muji unaojengwa juu ya mulima hauwezi kufichama.
15
Hakuna mutu anayewakisha taa na kuiweka chini ya kitunga, lakini anaiweka juu ya kinara kusudi iwaangazie wote wanaokuwa ndani ya nyumba.
16
Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.
17
“Musizani kama nilikuja kuvunja Sheria ya Musa au mafundisho ya manabii. Mimi sikukuja kuvunja, lakini kukamilisha.
18
Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.
19
Ni kwa hiyo mutu yeyote atakayevunja hata amri moja inayokuwa ndogo kuliko zingine zote, na kuwafundisha watu wengine kufanya kama yeye, huyu atahesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni. Lakini yule atakayezishika na kuzifundisha wengine, huyu atahesabiwa kuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.
20
Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.
21
“Mumesikia kwamba babu zenu waliambiwa: ‘Usiue; mutu yeyote anayeua anapaswa kuhukumiwa.’
22
Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.
23
Basi kama ukienda kumutolea Mungu sadaka juu ya mazabahu na pale ukikumbuka kwamba ndugu yako yuko na neno juu yako,
24
uache sadaka yako pale mbele ya mazabahu na uende kwanza kusikilizana naye. Na kisha urudie na kutoa sadaka yako.
25
“Kama mutu akikushitaki, upatane naye upesi wakati mungali katika njia kwenda kwenye tribinali. Kama si vile, yule anayekushitaki atakutoa kwa mwamuzi, naye mwamuzi atakupeleka kwa askari, nawe utatupwa katika kifungo.
26
Kweli ninakuambia: hautatoka mule mpaka utakapomaliza kulipa sengi ya mwisho.
27
“Mumesikia kwamba imesemwa: ‘Usizini.’
28
Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemwangalia mwanamuke kwa kumutamani, amekwisha kuzini naye ndani ya moyo wake.
29
Basi kama jicho lako la kuume likikukosesha, uliongoe na kulitupa mbali. Ni heri kwako kupoteza kiungo chako kimoja kuliko mwili wako wote muzima kutupwa katika jehenamu.
30
Na kama mukono wako wa kuume ukikukosesha, uukate na kuutupa mbali. Ni heri kwako kupoteza kiungo chako kimoja kuliko mwili wako wote muzima kutupwa katika jehenamu.
31
“Na zaidi ya hii imesemwa: ‘Kila mutu anayemufukuza muke wake amupe barua ya kuachana naye.’
32
Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayeachana na muke wake, isipokuwa tu kwa sababu ya uzinzi, anamufanya muke yule kuwa muzinzi kama akiolewa tena. Na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa, anazini vilevile.
33
“Mumesikia vilevile kwamba babu zenu waliambiwa hivi: ‘Usifanye viapo vya uongo, lakini sherti utimize viapo vyako mbele ya Bwana.’
34
Lakini mimi ninawaambia: musiape hata kidogo kwa jina la mbingu, kwa maana ni kiti cha kifalme cha Mungu;
35
wala kwa jina la dunia, kwa maana ni kiti chake cha kupumzishia miguu; wala kwa jina la Yerusalema, kwa maana ni muji wa Mufalme mukubwa.
36
Mutu asiape akitaja hata kichwa chake mwenyewe, kwa maana hawezi kugeuza hata unywele wake mumoja kuwa mweupe au mweusi.
37
Lakini munaposema, museme tu: ‘Ndiyo,’ au ‘Hapana,’ kwa maana maneno yanayosemwa zaidi ya hayo yanatoka kwa yule mwovu Shetani.
38
“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Jicho kwa jicho, na jino kwa jino.’
39
Lakini mimi ninawaambia: musirudishe mabaya kwa mabaya. Kama mutu akikupiga kofi kwa shavu la kuume, umugeuzie shavu la kushoto vilevile.
40
Kama mutu akitaka kukushitaki kusudi akunyanganye shemizi yako, umwachie koti yako vilevile.
41
Kama mutu anayetumwa na wakubwa akikulazimisha kubeba muzigo kilometre moja, uubebe hata kilometre mbili.
42
Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.
43
“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Umupende mwenzako, lakini umuchukie adui yako.’
44
Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.
45
Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.
46
Zawadi gani mutapata kutoka kwa Mungu, kama mukiwapenda tu wenye kuwapenda? Hata walipishaji wa kodi wanaokuwa wakorofi wanatendeana vile!
47
Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!
48
Basi mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni anavyokuwa mukamilifu.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 6 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28