bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Zechariah 2
Zechariah 2
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 3 →
1
Katika maono mengine, niliona pembe ine.
2
Nami nikamwuliza yule malaika aliyezungumuza nami: Pembe hizi zina maana gani? Yeye akanijibu: Pembe hizi zina maana ya yale mataifa ambayo yaliwatawanya watu wa Yuda, Israeli na Yerusalema.
3
Kisha, Yawe akanionyesha wafuachuma wane.
4
Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.
5
Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.
6
Basi, nikamwuliza: Unakwenda wapi? Naye akanijibu: Ninakwenda kuupima urefu na upana wa Yerusalema.
7
Yule malaika aliyezungumuza nami akaenda kukutana na malaika mwingine ambaye alikuwa anakuja kwake.
8
Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.
9
Yawe anasema kwamba yeye mwenyewe atakuwa ukuta wa moto kwa kuulinda muji huo pande zote, naye atakaa mule kwa utukufu wake.
10
Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.
11
Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!
12
Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.
13
Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.
14
Yawe anasema hivi: Enyi watu wa Sayuni, muimbe na kufurahi kwa maana ninakuja na kukaa kati yenu.
15
Mataifa mengi yatajiunga nami Yawe, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yenu. Halafu mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma kwenu.
16
Watu wa Yuda watakuwa tena mali ya pekee ya Yawe katika inchi takatifu, na Yerusalema itakuwa tena muji wake aliouchagua.
17
Enyi wanadamu wote, munyamaze mbele ya Yawe, maana, yeye anakuja kutoka makao yake matakatifu.
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 3 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14