bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
/
Psalms 119
Psalms 119
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
← Chapter 118
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 53
Chapter 54
Chapter 55
Chapter 56
Chapter 57
Chapter 58
Chapter 59
Chapter 60
Chapter 61
Chapter 62
Chapter 63
Chapter 64
Chapter 65
Chapter 66
Chapter 67
Chapter 68
Chapter 69
Chapter 70
Chapter 71
Chapter 72
Chapter 73
Chapter 74
Chapter 75
Chapter 76
Chapter 77
Chapter 78
Chapter 79
Chapter 80
Chapter 81
Chapter 82
Chapter 83
Chapter 84
Chapter 85
Chapter 86
Chapter 87
Chapter 88
Chapter 89
Chapter 90
Chapter 91
Chapter 92
Chapter 93
Chapter 94
Chapter 95
Chapter 96
Chapter 97
Chapter 98
Chapter 99
Chapter 100
Chapter 101
Chapter 102
Chapter 103
Chapter 104
Chapter 105
Chapter 106
Chapter 107
Chapter 108
Chapter 109
Chapter 110
Chapter 111
Chapter 112
Chapter 113
Chapter 114
Chapter 115
Chapter 116
Chapter 117
Chapter 118
Chapter 119
Chapter 120
Chapter 121
Chapter 122
Chapter 123
Chapter 124
Chapter 125
Chapter 126
Chapter 127
Chapter 128
Chapter 129
Chapter 130
Chapter 131
Chapter 132
Chapter 133
Chapter 134
Chapter 135
Chapter 136
Chapter 137
Chapter 138
Chapter 139
Chapter 140
Chapter 141
Chapter 142
Chapter 143
Chapter 144
Chapter 145
Chapter 146
Chapter 147
Chapter 148
Chapter 149
Chapter 150
Chapter 120 →
1
Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana.
2
Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.
3
Naam, hawakutenda ubatili, Wamekwenda katika njia zake.
4
Wewe umetuamuru mausia yako, Ili sisi tuyatii sana.
5
Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako.
6
Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.
7
Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako
8
Nitazitii amri zako, Usiniache kabisa
9
Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.
10
Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
11
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
12
Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako.
13
Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako.
14
Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi.
15
Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako.
16
Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.
17
Umtendee mtumishi wako ukarimu, Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako.
18
Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako.
19
Mimi ni mgeni katika nchi, Usinifiche maagizo yako.
20
Roho yangu imepondeka kwa kutamani Hukumu zako kila wakati.
21
Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako.
22
Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.
23
Wakuu nao waliketi wakaninena, Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako.
24
Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.
25
Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, Unihuishe sawasawa na neno lako.
26
Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako.
27
Unifahamishe njia ya mausia yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.
28
Nafsi yangu imeyeyuka kwa uzito, Unitie nguvu sawasawa na neno lako.
29
Uniondolee njia ya uongo, Unineemeshe kwa sheria yako.
30
Nimeichagua njia ya uaminifu, Na kuziweka hukumu zako mbele yangu.
31
Nimeambatana na shuhuda zako, Ee Bwana, usiniaibishe.
32
Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako, Utakaponikunjua moyo wangu.
33
Ee Bwana, unifundishe njia ya amri zako, Nami nitaishika hata mwisho.
34
Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote.
35
Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, Kwa maana nimependezwa nayo.
36
Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa.
37
Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako.
38
Umthibitishie mtumishi wako ahadi yako, Inayohusu kicho chako.
39
Uniondolee laumu niiogopayo, Maana hukumu zako ni njema.
40
Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.
41
Ee Bwana, fadhili zako zinifikie na mimi, Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako.
42
Nami nitamjibu neno anilaumuye, Kwa maana nalitumainia neno lako.
43
Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, Maana nimezingojea hukumu zako.
44
Nami nitaitii sheria yako daima, Naam, milele na milele.
45
Nami nitakwenda panapo nafasi, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
46
Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu.
47
Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda.
48
Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako.
49
Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako, Kwa sababu umenitumainisha.
50
Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha.
51
Wenye kiburi wamenidharau mno, Sikujiepusha na sheria zako.
52
Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee Bwana, nikajifariji.
53
Ghadhabu imenishika kwa sababu ya wasio haki, Waiachao sheria yako.
54
Amri zako zimekuwa nyimbo zangu, Katika nyumba ya ugeni wangu.
55
Wakati wa usiku nimelikumbuka jina lako, Ee Bwana, nikaitii sheria yako.
56
Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako.
57
Bwana ndiye aliye fungu langu, Nimesema kwamba nitayatii maneno yake.
58
Nimekuomba radhi kwa moyo wangu wote, Unifadhili sawasawa na ahadi yako.
59
Nalizitafakari njia zangu, Na miguu yangu nalizielekezea shuhuda zako.
60
Nalifanya haraka wala sikukawia, Kuyatii maagizo yako.
61
Kamba za wasio haki zimenifunga, Sikuisahau sheria yako.
62
Katikati ya usiku nitaamka nikushukuru, Kwa sababu ya hukumu zako za haki.
63
Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.
64
Bwana, dunia imejaa fadhili zako, Unifundishe amri zako.
65
Umemtendea mema mtumishi wako, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
66
Unifundishe akili na maarifa, Maana nimeyaamini maagizo yako.
67
Kabla sijateswa mimi nalipotea, Lakini sasa nimelitii neno lako.
68
Wewe U mwema na mtenda mema, Unifundishe amri zako.
69
Wenye kiburi wamenizulia uongo, Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako.
70
Mioyo yao imenenepa kama shahamu, Mimi nimeifurahia sheria yako.
71
Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, Nipate kujifunza amri zako.
72
Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.
73
Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza, Unifahamishe nikajifunze maagizo yako.
74
Wakuchao na wanione na kufurahi, Kwa sababu nimelingojea neno lako.
75
Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, Ee Bwana, na kwa uaminifu umenitesa.
76
Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu, Sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
77
Rehema zako zinijie nipate kuishi, Maana sheria yako ni furaha yangu.
78
Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako.
79
Wakuchao na wanirudie, Nao watazijua shuhuda zako.
80
Moyo wangu na uwe mkamilifu katika amri zako, Nisije mimi nikaaibika.
81
Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelingojea neno lako.
82
Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nisemapo, Lini utakaponifariji?
83
Maana nimekuwa kama kiriba katika moshi, Sikuzisahau amri zako.
84
Siku za mtumishi wako ni ngapi, Lini utakapowahukumu wale wanaonifuatia?
85
Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, Ambao hawaifuati sheria yako.
86
Maagizo yako yote ni amini, Wananifuatia bure, unisaidie.
87
Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi, Lakini sikuyaacha mausia yako.
88
Unihuishe kwa fadhili zako, Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako.
89
Ee Bwana, neno lako lasimama Imara mbinguni hata milele.
90
Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.
91
Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, Maana vitu vyote ni watumishi wako.
92
Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu, Hapo ningalipotea katika taabu zangu.
93
Hata milele sitayasahau maagizo yako, Maana kwa hayo umenihuisha.
94
Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako.
95
Wasio haki wameniotea ili kunipoteza, Nitazitafakari shuhuda zako.
96
Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, Bali agizo lako ni pana mno.
97
Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.
98
Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, Kwa maana ninayo sikuzote.
99
Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
100
Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.
101
Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya, Ili nilitii neno lako.
102
Sikujiepusha na hukumu zako, Maana Wewe mwenyewe umenifundisha.
103
Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu.
104
Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.
105
Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
106
Nimeapa nami nitaifikiliza, Kuzishika hukumu za haki yako.
107
Nimeteswa mno; Ee Bwana, unihuishe sawasawa na neno lako.
108
Ee Bwana, uziridhie sadaka za kinywa changu, Na kunifundisha hukumu zako.
109
Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, Lakini sheria yako sikuisahau.
110
Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sikuikosa njia ya mausia yako.
111
Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, Maana ndizo changamko la moyo wangu.
112
Nimeuelekeza moyo wangu nizitende amri zako, Daima, naam, hata milele.
113
Watu wa kusita-sita nawachukia, Lakini sheria yako naipenda.
114
Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea.
115
Enyi watenda mabaya, ondokeni kwangu, Niyashike maagizo ya Mungu wangu.
116
Unitegemeze sawasawa na ahadi yako, nikaishi, Wala usiniache niyaaibikie matumaini yangu.
117
Unisaidie nami nitakuwa salama, Nami nitaziangalia amri zako daima.
118
Umewakataa wote wazikosao amri zako, Kwa maana hila zao ni uongo.
119
Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka, Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako.
120
Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe, Nami ninaziogopa hukumu zako.
121
Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea.
122
Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, Wenye kiburi wasinionee.
123
Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako, Na ahadi ya haki yako.
124
Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe.
125
Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako.
126
Wakati umewadia Bwana atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako.
127
Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi.
128
Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.
129
Shuhuda zako ni za ajabu, Ndiyo maana roho yangu imezishika.
130
Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.
131
Nalifunua kinywa changu nikatweta, Maana naliyatamani maagizo yako.
132
Unigeukie, unirehemu mimi, Kama iwahusuvyo walipendao jina lako.
133
Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako, Uovu usije ukanimiliki.
134
Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu, Nipate kuyashika mausia yako.
135
Umwangazie mtumishi wako uso wako, Na kunifundisha amri zako.
136
Macho yangu yachuruzika mito ya maji, Kwa sababu hawaitii sheria yako.
137
Ee Bwana, Wewe ndiwe mwenye haki, Na hukumu zako ni za adili.
138
Umeziagiza shuhuda zako kwa haki, Na kwa uaminifu mwingi.
139
Juhudi yangu imeniangamiza, Maana watesi wangu wameyasahau maneno yako.
140
Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.
141
Mimi ni mdogo, nadharauliwa, Lakini siyasahau mausia yako.
142
Haki yako ni haki ya milele, Na sheria yako ni kweli.
143
Taabu na dhiki zimenipata, Maagizo yako ni furaha yangu.
144
Haki ya shuhuda zako ni ya milele, Unifahamishe, nami nitaishi.
145
Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee Bwana, uitike; Nitazishika amri zako.
146
Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako.
147
Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
148
Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku, Ili kuitafakari ahadi yako.
149
Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150
Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, Wamekwenda mbali na sheria yako.
151
Ee Bwana, Wewe U karibu, Na maagizo yako yote ni kweli.
152
Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.
153
Uyaangalie mateso yangu, uniokoe, Maana sikuisahau sheria yako.
154
Unitetee na kunikomboa, Unihuishe sawasawa na ahadi yako.
155
Wokovu u mbali na wasio haki, Kwa maana hawajifunzi amri zako.
156
Ee Bwana, rehema zako ni nyingi, Unihuishe sawasawa na hukumu zako.
157
Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
158
Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako.
159
Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na fadhili zako.
160
Jumla ya neno lako ni kweli, Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.
161
Wakuu wameniudhi bure, Ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
162
Naifurahia ahadi yako, Kama apataye mateka mengi.
163
Nimeuchukia uongo, umenikirihi, Sheria yako nimeipenda.
164
Mara saba kila siku nakusifu, Kwa sababu ya hukumu za haki yako.
165
Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.
166
Ee Bwana, nimeungojea wokovu wako, Na maagizo yako nimeyatenda.
167
Nafsi yangu imezishika shuhuda zako, Nami nazipenda mno.
168
Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.
169
Ee Bwana, kilio changu na kikukaribie, Unifahamishe sawasawa na neno lako.
170
Dua yangu na ifike mbele zako, Uniponye sawasawa na ahadi yako.
171
Midomo yangu na itoe sifa, Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.
172
Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako, Maana maagizo yako yote ni ya haki.
173
Mkono wako na uwe tayari kunisaidia, Maana nimeyachagua mausia yako.
174
Ee Bwana, nimeutamani wokovu wako, Na sheria yako ndiyo furaha yangu.
175
Nafsi yangu na iishi, ipate kukusifu, Na hukumu zako zinisaidie.
176
Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; Umtafute mtumishi wako; Kwa maana sikuyasahau maagizo yako.
← Chapter 118
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 53
Chapter 54
Chapter 55
Chapter 56
Chapter 57
Chapter 58
Chapter 59
Chapter 60
Chapter 61
Chapter 62
Chapter 63
Chapter 64
Chapter 65
Chapter 66
Chapter 67
Chapter 68
Chapter 69
Chapter 70
Chapter 71
Chapter 72
Chapter 73
Chapter 74
Chapter 75
Chapter 76
Chapter 77
Chapter 78
Chapter 79
Chapter 80
Chapter 81
Chapter 82
Chapter 83
Chapter 84
Chapter 85
Chapter 86
Chapter 87
Chapter 88
Chapter 89
Chapter 90
Chapter 91
Chapter 92
Chapter 93
Chapter 94
Chapter 95
Chapter 96
Chapter 97
Chapter 98
Chapter 99
Chapter 100
Chapter 101
Chapter 102
Chapter 103
Chapter 104
Chapter 105
Chapter 106
Chapter 107
Chapter 108
Chapter 109
Chapter 110
Chapter 111
Chapter 112
Chapter 113
Chapter 114
Chapter 115
Chapter 116
Chapter 117
Chapter 118
Chapter 119
Chapter 120
Chapter 121
Chapter 122
Chapter 123
Chapter 124
Chapter 125
Chapter 126
Chapter 127
Chapter 128
Chapter 129
Chapter 130
Chapter 131
Chapter 132
Chapter 133
Chapter 134
Chapter 135
Chapter 136
Chapter 137
Chapter 138
Chapter 139
Chapter 140
Chapter 141
Chapter 142
Chapter 143
Chapter 144
Chapter 145
Chapter 146
Chapter 147
Chapter 148
Chapter 149
Chapter 150
Chapter 120 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52
53
54
55
56
57
58
59
60
61
62
63
64
65
66
67
68
69
70
71
72
73
74
75
76
77
78
79
80
81
82
83
84
85
86
87
88
89
90
91
92
93
94
95
96
97
98
99
100
101
102
103
104
105
106
107
108
109
110
111
112
113
114
115
116
117
118
119
120
121
122
123
124
125
126
127
128
129
130
131
132
133
134
135
136
137
138
139
140
141
142
143
144
145
146
147
148
149
150