bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
/
Psalms 78
Psalms 78
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
← Chapter 77
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 53
Chapter 54
Chapter 55
Chapter 56
Chapter 57
Chapter 58
Chapter 59
Chapter 60
Chapter 61
Chapter 62
Chapter 63
Chapter 64
Chapter 65
Chapter 66
Chapter 67
Chapter 68
Chapter 69
Chapter 70
Chapter 71
Chapter 72
Chapter 73
Chapter 74
Chapter 75
Chapter 76
Chapter 77
Chapter 78
Chapter 79
Chapter 80
Chapter 81
Chapter 82
Chapter 83
Chapter 84
Chapter 85
Chapter 86
Chapter 87
Chapter 88
Chapter 89
Chapter 90
Chapter 91
Chapter 92
Chapter 93
Chapter 94
Chapter 95
Chapter 96
Chapter 97
Chapter 98
Chapter 99
Chapter 100
Chapter 101
Chapter 102
Chapter 103
Chapter 104
Chapter 105
Chapter 106
Chapter 107
Chapter 108
Chapter 109
Chapter 110
Chapter 111
Chapter 112
Chapter 113
Chapter 114
Chapter 115
Chapter 116
Chapter 117
Chapter 118
Chapter 119
Chapter 120
Chapter 121
Chapter 122
Chapter 123
Chapter 124
Chapter 125
Chapter 126
Chapter 127
Chapter 128
Chapter 129
Chapter 130
Chapter 131
Chapter 132
Chapter 133
Chapter 134
Chapter 135
Chapter 136
Chapter 137
Chapter 138
Chapter 139
Chapter 140
Chapter 141
Chapter 142
Chapter 143
Chapter 144
Chapter 145
Chapter 146
Chapter 147
Chapter 148
Chapter 149
Chapter 150
Chapter 79 →
1
Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.
2
Na nifunue kinywa changu kwa mithali, Niyatamke mafumbo ya kale.
3
Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, Ambayo baba zetu walituambia.
4
Hayo hatutawaficha wana wao, Huku tukiwaambia kizazi kingine, Sifa za Bwana, na nguvu zake, Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.
5
Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, Na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu Wawajulishe wana wao,
6
Ili kizazi kingine wawe na habari, Ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao
7
Wamwekee Mungu tumaini lao. Wala wasiyasahau matendo ya Mungu, Bali wazishike amri zake.
8
Naam, wasiwe kama baba zao, Kizazi cha ukaidi na uasi. Kizazi kisichojitengeneza moyo, Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.
9
Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde, Walirudi nyuma siku ya vita.
10
Hawakulishika agano la Mungu; Wakakataa kuenenda katika sheria yake;
11
Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.
12
Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani.
13
Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.
14
Akawaongoza kwa wingu mchana, Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
15
Akapasua miamba jangwani; Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
16
Akatokeza na vijito gengeni, Akatelemsha maji kama mito.
17
Lakini wakazidi kumtenda dhambi, Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
18
Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
19
Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
20
Tazama, aliupiga mwamba; Maji yakabubujika, ikafurika mito. Pia aweza kutupa chakula? Atawaandalia watu wake nyama?
21
Hivyo Bwana aliposikia akaghadhibika; Moto ukawashwa juu ya Yakobo, Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
22
Kwa kuwa hawakumwamini Mungu, Wala hawakuutumainia wokovu wake.
23
Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni;
24
Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni.
25
Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
26
Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni; Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
27
Akawanyeshea nyama kama mavumbi, Na ndege wenye mbawa, Kama mchanga wa bahari.
28
Akawaangusha kati ya matuo yao, Pande zote za maskani zao.
29
Wakala wakashiba sana; Maana aliwaletea walivyovitamani;
30
Hawakuachana na matakwa yao. Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao
31
Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli.
32
Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33
Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha.
34
Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii.
35
Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao.
36
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, Wakamwambia uongo kwa ndimi zao.
37
Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38
Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.
39
Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.
40
Walimwasi jangwani mara ngapi? Na kumhuzunisha nyikani!
41
Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli.
42
Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.
43
Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani.
44
Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa.
45
Aliwapelekea mainzi wakawala, Na vyura wakawaharibu.
46
Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige kazi yao.
47
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu.
48
Akaacha ng'ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, Na makundi yao kwa umeme.
49
Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya.
50
Akiifanyizia njia hasira yake; Wala hakuziepusha roho zao na mauti, Bali aliiachia tauni uhai wao;
51
Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu.
52
Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani.
53
Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunikiza adui zao.
54
Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume.
55
Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao.
56
Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake.
57
Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa.
58
Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
59
Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.
60
Akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
61
Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
62
Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga; Akaughadhibikia urithi wake.
63
Moto ukawala vijana wao, Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64
Makuhani wao walianguka kwa upanga, Wala wajane wao hawakuomboleza.
65
Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi, Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo;
66
Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, Akawatia aibu ya milele.
67
Ila akaikataa hema ya Yusufu; Wala hakuichagua kabila ya Efraimu.
68
Bali aliichagua kabila ya Yuda, Mlima Sayuni alioupenda.
69
Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele.
70
Akamchagua Daudi, mtumishi wake, Akamwondoa katika mazizi ya kondoo.
71
Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa, Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake.
72
Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake.
← Chapter 77
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 53
Chapter 54
Chapter 55
Chapter 56
Chapter 57
Chapter 58
Chapter 59
Chapter 60
Chapter 61
Chapter 62
Chapter 63
Chapter 64
Chapter 65
Chapter 66
Chapter 67
Chapter 68
Chapter 69
Chapter 70
Chapter 71
Chapter 72
Chapter 73
Chapter 74
Chapter 75
Chapter 76
Chapter 77
Chapter 78
Chapter 79
Chapter 80
Chapter 81
Chapter 82
Chapter 83
Chapter 84
Chapter 85
Chapter 86
Chapter 87
Chapter 88
Chapter 89
Chapter 90
Chapter 91
Chapter 92
Chapter 93
Chapter 94
Chapter 95
Chapter 96
Chapter 97
Chapter 98
Chapter 99
Chapter 100
Chapter 101
Chapter 102
Chapter 103
Chapter 104
Chapter 105
Chapter 106
Chapter 107
Chapter 108
Chapter 109
Chapter 110
Chapter 111
Chapter 112
Chapter 113
Chapter 114
Chapter 115
Chapter 116
Chapter 117
Chapter 118
Chapter 119
Chapter 120
Chapter 121
Chapter 122
Chapter 123
Chapter 124
Chapter 125
Chapter 126
Chapter 127
Chapter 128
Chapter 129
Chapter 130
Chapter 131
Chapter 132
Chapter 133
Chapter 134
Chapter 135
Chapter 136
Chapter 137
Chapter 138
Chapter 139
Chapter 140
Chapter 141
Chapter 142
Chapter 143
Chapter 144
Chapter 145
Chapter 146
Chapter 147
Chapter 148
Chapter 149
Chapter 150
Chapter 79 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52
53
54
55
56
57
58
59
60
61
62
63
64
65
66
67
68
69
70
71
72
73
74
75
76
77
78
79
80
81
82
83
84
85
86
87
88
89
90
91
92
93
94
95
96
97
98
99
100
101
102
103
104
105
106
107
108
109
110
111
112
113
114
115
116
117
118
119
120
121
122
123
124
125
126
127
128
129
130
131
132
133
134
135
136
137
138
139
140
141
142
143
144
145
146
147
148
149
150