bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
/
Jeremiah 36
Jeremiah 36
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 37 →
1
Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa BWANA kusema:
2
“Chukua kitabu na uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
3
Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo kila mmoja wao atageuka kutoka katika njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
4
Hivyo Yeremia akamwita Baruki mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema BWANA, Baruki akayaandika katika kitabu.
5
Kisha Yeremia akamwambia Baruki, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la BWANA.
6
Basi wewe nenda katika nyumba ya BWANA siku ya kufunga na uwasomee watu maneno ya BWANA kutoka katika kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka kwenye miji yao.
7
Labda wataomba na kusihi mbele za BWANA na kila mmoja atageuka kutoka katika njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na BWANA ni kubwa.”
8
Baruki mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya, katika Hekalu la BWANA alisoma maneno ya BWANA kutoka katika kile kitabu.
9
Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za BWANA ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
10
Kutoka katika chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruki akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la BWANA maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
11
Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya BWANA kutoka kwenye kile kitabu,
12
alishuka kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote, yaani: Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania na maafisa wengine wote.
13
Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruki akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
14
maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruki, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruki mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
15
Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruki akawasomea kile kitabu.
16
Walipoyasikia maneno haya yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruki, “Ni lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
17
Kisha wakamwuliza Baruki, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
18
Baruki akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
19
Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruki, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu ye yote asijue mahali mlipo.”
20
Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
21
Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu na Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
22
Ulikuwa mwezi wa tisa na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
23
Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni hadi kitabu chote kikateketea.
24
Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yo yote wala hawakuyararua mavazi yao.
25
Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu lakini hakuwasikiliza.
26
Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruki na nabii Yeremia. Lakini BWANA alikuwa amewaficha.
27
Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruki aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la BWANA lilimjia Yeremia likisema:
28
“Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
29
Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo BWANA: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
30
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo BWANA kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu ye yote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi, maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
31
Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao, nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’ ”
32
Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruki mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruki akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto na maneno mengine mengi yanayofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 37 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52