bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Samuel 18
1 Samuel 18
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 19 →
1
Saulo alipomaliza kuzungumuza na Daudi, Yonatani mwana wa Saulo alivutwa sana na Daudi, akamupenda kwa moyo wake wote kama alivyojipenda yeye mwenyewe.
2
Tangu siku ile, Saulo akamutwaa Daudi katika nyumba yake, hakumuruhusu kurudi kwenye nyumba ya baba yake.
3
Kwa sababu Yonatani alimupenda Daudi kama roho yake, alifanya agano naye.
4
Alivua nguo aliyovaa na kumupa Daudi pamoja na silaha zake, hata upanga, upinde na mukaba wake.
5
Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.
6
Waaskari walipokuwa wanarudi kwenye nyumba, pamoja na Daudi kisha kumwua yule Mufilistini, wanawake kutoka kila muji katika Israeli walitoka kwenda kumupokea mufalme Saulo. Wanawake nao walikuwa wanaimba nyimbo za furaha, wakipiga matari na vinubi.
7
Vilevile walikuwa wanacheza na kuimba nyimbo za kuitikiana hivi: “Saulo ameua maelfu yake, na Daudi ameua elfu yake makumi.”
8
Saulo hakupendezwa na maneno ya wimbo huo. Akakasirika sana. Akasema: “Wamemupa Daudi elfu makumi, lakini mimi wamenipa maelfu tu. Linalobakia ni kumupa Daudi ufalme.”
9
Tangu siku hiyo, Saulo akakuwa anamusikilia Daudi wivu.
10
Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.
11
Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.
12
Saulo alikuwa anamwogopa Daudi kwa sababu Yawe alikuwa pamoja naye, lakini Yawe alikuwa amemwacha Saulo.
13
Hivyo, Saulo akamwondoa na kumufanya kiongozi wa waaskari elfu moja. Naye Daudi akawaongoza vyema katika vita.
14
Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.
15
Saulo alipoona kufanikiwa kwa Daudi, akakuwa anamwogopa.
16
Lakini watu wote wa Israeli na Yuda walimupenda Daudi, maana ndiye aliwaongoza vizuri katika vita na kuwarudisha na mafanikio.
17
Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.
18
Daudi akamwambia Saulo: “Mimi ni nani hata mufalme akuwe baba mukwe wangu? Ukoo wangu wenyewe na hata jamaa ya baba yangu si kitu katika Israeli.”
19
Lakini, wakati ule ambapo Merabu binti ya Saulo angeoeshwa kwa Daudi, alioeshwa kwa Adrieli kutoka muji wa Mehola.
20
Hata hivyo, Mikali binti mwingine wa Saulo alimupenda Daudi. Saulo alipoambiwa habari ile alifurahi sana.
21
Saulo alifikiri: “Ngoja nitamutoa Mikali kusudi akuwe mutego kwake. Na bila shaka Wafilistini watamwua.” Hivyo Saulo akamwambia Daudi kwa mara ya pili: “Sasa nitakuwa baba mukwe wako.”
22
Halafu Saulo aliwaamuru watumishi wake akisema: “Museme na Daudi kwa siri na kumwambia: ‘Mufalme anapendezwa sana nawe, hata watumishi wake vilevile wote wanakupenda’. Hivyo, sasa ukubali kuwa mukwe wa mufalme.”
23
Basi, watumishi hao wa Saulo walimwambia Daudi maneno hayo kwa siri, naye akawaambia: “Munazani mufalme kuwa baba mukwe wangu ni jambo dogo? Mimi ni mutu masikini na wa hali ya chini.”
24
Wale watumishi walimwelezea Saulo kama vile Daudi alivyosema.
25
Saulo akawaambia: “Mumwambie Daudi hivi: ‘Kile ambacho mufalme anataka kama vile mali kwa binti yake ni magovi mia moja ya Wafilistini, kusudi ajilipize kisasi kwa waadui zake.’ ” Hivi ndivyo Saulo alivyopanga kusudi Daudi auawe na Wafilistini.
26
Wale watumishi walipomwelezea Daudi yale mapenzi ya Saulo, Daudi alifurahi kwamba mufalme atakuwa baba mukwe wake. Mbele ya siku ya arusi,
27
Daudi na watu wake walikwenda, wakawaua Wafilistini mia mbili na kuyatwaa magovi yao mpaka kwa mufalme Saulo. Hapo akamuhesabilia hesabu kamili kusudi mufalme akuwe baba mukwe wa Daudi. Hivyo, Saulo akamupatia Daudi binti yake Mikali akuwe muke wake.
28
Lakini Saulo alipoona wazi kwamba Yawe alikuwa pamoja na Daudi, na kwamba Mikali binti yake alimupenda sana Daudi,
29
alizidi kumwogopa Daudi. Saulo akakuwa adui wa Daudi siku zote.
30
Waaskari wa Wafilistini walikwenda kupigana na Waisraeli, lakini kila mara walipopigana vita, Daudi alipata ushindi kuliko watumishi wa Saulo. Hivyo jina la Daudi likazidi kusifiwa sana.
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 19 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31