bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Samuel 27
1 Samuel 27
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 26
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 28 →
1
Daudi akajisemesha ndani ya moyo: “Siku moja, Saulo ataniangamiza. Jambo zuri kwangu ni kukimbilia katika inchi ya Wafilistini. Saulo atakata tamaa kunitafuta ndani ya mipaka ya inchi ya Israeli, nami nitakuwa salama kutoka katika mikono yake.”
2
Kwa hiyo, mara moja Daudi na watu wake mia sita wakaenda kwa Akisi mwana wa Maoki, mufalme wa Gati.
3
Daudi na watu wake pamoja na jamaa yake wakaishi na Akisi kule Gati. Daudi alikuwa na wake wawili: Ahinoamu kutoka Yezereheli na Abigaili mujane wa Nabali kutoka muji wa Karmeli.
4
Saulo aliposikia kwamba Daudi amekimbilia Gati, hakumufuata tena.
5
Siku moja, Daudi akamwambia Akisi: “Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba unipe muji mumoja katika inchi yako kusudi ukuwe pahali pangu pa kuishi. Hakuna faida kwangu kuishi nawe katika muji huu wa kifalme.”
6
Siku hiyo, Akisi akamupa muji wa Ziklagi. Kwa hiyo, tangu siku hiyo muji wa Ziklagi ukakuwa mali ya wafalme wa Yuda.
7
Daudi aliishi katika inchi ya Wafilistini kwa muda wa mwaka mumoja na miezi mine.
8
Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.
9
Daudi aliipiga inchi hiyo pasipo kuacha mutu yeyote muzima, akuwe mwanaume au mwanamuke, akateka kondoo, ngombe, punda, ngamia na nguo; kisha akarudi na kufika kwa Akisi.
10
Akisi alipomwuliza: “Leo mashambulizi yako yalikuwa juu ya nani?” Daudi alimwambia: “Juu ya Negebu ya Yuda” au “Juu ya Negebu ya Wayerameli” au “Juu ya Negebu ya Wakeni”.
11
Daudi hakumwacha mutu yeyote muzima akuwe mwanaume au mwanamuke kusudi aletwe Gati; alifikiri ndani ya moyo: “Wanaweza kueleza juu yetu na kusema: ‘Daudi alifanya kitendo hiki na kile.’ ” Hivyo ndivyo Daudi alivyozoea kutenda wakati wote alipoishi katika inchi ya Wafilistini.
12
Kwa hiyo, Akisi alimusadiki Daudi, akifikiri: “Wanainchi wenzake Waisraeli hawamupendi kabisa. Kwa hiyo, atanitumikia maisha yake yote.”
← Chapter 26
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 28 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31