bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Samuel 21
1 Samuel 21
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 22 →
1
Daudi akasimama na kwenda zake, naye Yonatani akarudi katika muji.
2
Daudi alikwenda kwa kuhani Ahimeleki kule Noba. Ahimeleki akaenda kumupokea akiwa anatetemeka, akamwuliza: “Kwa nini umekuja hapa peke yako?”
3
Daudi akamujibu: “Niko hapa kutokana na amri ya mufalme. Aliniambia nisimwelezee mutu yeyote juu ya kile ambacho amenituma. Nimeagana na watu wangu kwamba tukutane pahali fulani.
4
Uko na kitu chochote? Ninakuomba mikate mitano au chochote kinachokuwa.”
5
Kuhani Ahimeleki akamwambia: “Hapa sina mukate wa kawaida. Niko tu na ile mikate mitakatifu. Munaweza kupewa mikate hiyo ikiwa watu wako wamejitenga na wanawake siku hizi.”
6
Daudi akamwambia: “Kwa hakika, ninapokwenda kwa ajili ya shuguli kubwa, wanawake wanatengwa mbali nasi! Ikiwa miili ya vijana wangu inakuwa mitakatifu na safi tunapokuwa kwenye shuguli za kawaida, basi, si zaidi katika shuguli hii kubwa?”
7
Kwa hiyo kuhani Ahimeleki akamupa mikate mitakatifu, maana hapakukuwa mikate mingine isipokuwa ile ambayo inaondolewa mbele ya Yawe na kubadilishwa na mikate mipya kutoka kwenye jiko.
8
Basi siku ile pale kulikuwa mutumishi mumoja wa Saulo ambaye alikuwa amezuiliwa mbele ya Yawe. Mutumishi yule aliitwa Doegi Mwedomu, aliyekuwa musimamizi wa wachungaji wa nyama wa Saulo.
9
Basi, Daudi akamwambia Ahimeleki: “Una upanga au mukuki ambao unaweza kunipatia? Kwa maana shuguli za mufalme zilinilazimisha niondoke haraka, nami niliondoka bila upanga wangu wala silaha nyingine yoyote.”
10
Ahimeleki akamujibu: “Upanga wa Goliati Mufilistini uliyemwua kwenye bonde la Ela uko nyuma ya efodi, unafungwa katika kitambaa. Ikiwa unataka kuukamata basi, uukamate maana hakuna upanga mwingine hapa.” Daudi akamwambia: “Hakuna upanga mwingine kama huo; unipe.”
11
Siku hiyo, Daudi alimukimbia Saulo, akaenda kwa mufalme Akisi wa Gati.
12
Watumishi wa mufalme wakamwambia Akisi: “Huyu si Daudi, mufalme wa inchi ya Israeli? Si huyu ambaye walikuwa wakiimbiana juu yake katika ngoma, wakisema: ‘Saulo ameua maelfu yake na Daudi ameua elfu makumi yake?’ ”
13
Daudi akafikiri sana juu ya maneno yale, akaanza kumwogopa sana Akisi mufalme wa Gati.
14
Hivyo, akabadilisha tabia yake, akijifanya mwenda-wazimu, akakuwa anakwaruzakwaruza kwenye milango ya muji, na kuacha mate yake yatiririke kwenye ndevu zake.
15
Akisi akawaambia watumishi wake: “Munajua kwamba mutu huyu ni mwenda-wazimu. Kwa nini mumemuleta kwangu?
16
Ninawahitaji wenda-wazimu zaidi? Kwa nini munaniletea mwenda-wazimu akuje kunisumbua na vitendo vya wenda-wazimu? Mutu huyu ataingia katika nyumba yangu?”
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 22 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31