bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Galatians 1
Galatians 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 2 →
1
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.
3
Tunawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
4
Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.
5
Mungu atukuzwe kwa milele na milele! Amina.
6
Ninashangaa sana kuona namna gani munageuka hivi upesi kwa kumwacha yule aliyewaita kwa njia ya neema ya Kristo na kufuata habari njema ya namna ingine.
7
Kwa kweli hakuna Habari Njema ingine, lakini kuko watu wanaowavuruga, wakitaka kugeuza Habari Njema ya Kristo.
8
Lakini kama sisi wenyewe au malaika kutoka mbinguni, akiwahubiri ninyi Habari Njema inayokuwa mbalimbali na ile tuliyowahubiri, alaaniwe!
9
Tumekwisha kuwaambia mambo haya zamani, nami ninayarudilia tena: mutu akiwahubiri habari njema inayokuwa mbalimbali na ile muliyopokea, alaaniwe!
10
Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.
11
Wandugu zangu, ninawajulisha kwamba Habari Njema ninayohubiri haikutungwa na mutu.
12
Sikuipokea kutoka kwa mutu wala sikuifundishwa na mutu, lakini ni Yesu Kristo aliyeifunua kwangu.
13
Mumesikia namna mwenendo wangu ulivyokuwa zamani, wakati nilipofuata dini ya Kiyuda. Munajua namna nilivyotesa kanisa la Mungu vikali sana na kujikaza kwa kuliharibu.
14
Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.
15
Lakini, Mungu aliyenichagua mbele sijazaliwa na kuniita kwa neema yake, alipendezwa
16
kumufunua Mwana wake kwangu, kusudi nihubiri Habari yake Njema kwa watu wa mataifa mengine. Na pale pale sikuomba shauri kwa mutu yeyote,
17
wala sikwenda Yerusalema kwa kuonana na wale waliokuwa mitume mbele yangu, lakini nikajiendea katika inchi ya Arabia. Kisha nikarudia tena Damasiki.
18
Kulipokwisha kupita miaka mitatu, nikaenda Yerusalema kusudi nipate kujuana na Petro, nami nikakaa kwake kwa muda wa siku kumi na tano.
19
Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.
20
Ninaapa mbele ya Mungu kuwa sisemi uongo katika maneno haya ninayowaandikia.
21
Nyuma ya pale nikaenda pande za jimbo la Suria na la Kilikia.
22
Katika siku zile makanisa ya Yudea yalikuwa hayajaniona kwa uso,
23
lakini yalikuwa yakisikia tu habari kwamba: “Yule aliyekuwa akitutesa zamani, sasa anahubiri habari za imani ile aliyokuwa akipotosha.”
24
Nao yalimusifu Mungu kwa ajili yangu.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6