bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Galatians 3
Galatians 3
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 4 →
1
Ee ninyi Wagalatia! Ninyi wajinga! Ni nani aliyewaloga? Habari juu ya kutundikwa kwa Yesu Kristo juu ya musalaba ilielezwa waziwazi mbele ya macho yenu.
2
Ninataka mujibu ulizo hili moja: mumepokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kushika Sheria au kwa sababu mumesikia na kuamini Habari Njema?
3
Namna gani mumekuwa wajinga hivi? Ninyi mumeanza mambo yote kwa nguvu za Roho wa Mungu, sasa munataka kuyatimiza kwa nguvu za kimwili?
4
Mambo yote yaliyowatokea ninyi, yalikuwa ya bure? Hakika hayakukuwa ya bure.
5
Mungu aliwajaza Roho wake na kufanya miujiza kati yenu kwa sababu munashika Sheria au kwa sababu munasikia na kuamini Habari Njema?
6
Hivyo “Abrahamu alimwamini Mungu, na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.”
7
Basi mutambue kwamba wazao wa kweli wa Abrahamu ni wale wanaokuwa wenye imani.
8
Vilevile Maandiko Matakatifu yalisema tangu zamani kwamba watu wa mataifa mengine watahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani yao. Kwa sababu Mungu alipasha kwanza Habari Njema hii kwa Abrahamu: “Kwa njia yako mataifa yote yatabarikiwa.”
9
Kufuatana na hiyo, Mungu atawabariki wote wanaoamini sawa vile alivyomubariki Abrahamu, mwenye imani.
10
Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”
11
Na zaidi ya hii ni wazi kwamba hakuna mutu anayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”
12
Na tena hakuna ushirika kati ya Sheria na imani. Lakini Maandiko Matakatifu yanasema: “Yule anayeshika maagizo ya Sheria hii ataishi kwa njia hiyo.”
13
Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”
14
Ilitendeka hivi kusudi kwa njia ya Yesu Kristo, baraka Mungu aliyoahidi kwa Abrahamu itolewe vilevile kwa watu wa mataifa mengine na hata sisi kwa njia ya imani, tupate kupokea yule Roho aliyeahidiwa na Mungu.
15
Wandugu, nitatumia mufano huu wa kawaida: mutu anapofanya agano kwa njia ya haki, hakuna mutu anayeweza kulivunja au kuongeza neno lingine juu yake.
16
Basi, Mungu alitoa ahadi kwa Abrahamu na uzao wake. Maandiko hayasemi kwamba alitoa ahadi zile kwa “wazao wake” kama vile angeitoa kwa watu wengi. Lakini yanasema kwamba “kwa uzao wako”, maana yake kwa mutu mumoja tu ndiye Kristo.
17
Mambo ninayotaka kusema ni haya: Mungu amekwisha kufanya agano kwa njia ya haki. Nayo Sheria iliyotokea miaka mia ine makumi tatu nyuma yake haiwezi kulivunja au kugeuza ile ahadi ya Mungu.
18
Lakini, kama zawadi ya Mungu inatokana na Sheria, basi, haiwezi kutokana tena na ahadi. Lakini kwa njia ya ahadi, Mungu ameonyesha wema wake kwa Abrahamu.
19
Basi Sheria iko na kazi gani? Ilisimamishwa nyuma kwa ajili ya kutambulisha makosa. Nayo ilipaswa kuendelea mpaka atakapokuja yule muzao wa Abrahamu ambaye Mungu alikuwa ameahidi. Sheria hii ilitangazwa na malaika kwa njia ya mupatanishi.
20
Lakini ikiwa jambo linaelekea mutu mumoja tu, si lazima kuwa na mupatanishi; na Mungu ni mumoja tu.
21
Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.
22
Lakini Maandiko Matakatifu yanasema kwamba watu wote wako chini ya utumwa wa zambi, kusudi zawadi iliyoahidiwa na Mungu itolewe kwa wale wanaoamini kwa njia ya imani yao katika Yesu Kristo.
23
Wakati wa imani ulipokuwa haujatokea, tulichungwa na Sheria, kama vile wafungwa, tukingojea mpaka imani ile ifunuliwe.
24
Hivi Sheria ilikuwa kama mwangalizi wetu mpaka Kristo alipofika, kusudi tuhesabiwe haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani.
25
Lakini tangia kufika kwa imani, sisi hatuko tena chini ya uangalizi ule.
26
Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.
27
Hivi, ninyi wote mulioungana na Yesu Kristo, kwa njia ya kubatizwa, ni kama vile mumevaa Kristo.
28
Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.
29
Kama ninyi ni watu wa Kristo, basi, ninyi ni wazao wa Abrahamu, ninyi mutakuwa warizi sawa vile Mungu alivyoahidi.
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6