bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Galatians 2
Galatians 2
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 3 →
1
Kulipokwisha kupita miaka kumi na mine, nikarudia Yerusalema pamoja na Barnaba; nami nilikuwa pamoja na Tito vilevile.
2
Nilienda kule kufuatana na agizo nililopata katika maono. Halafu nikakusanyika na waongozi kwa upekee. Nikawaelezea Habari Njema ninayohubiri kati ya mataifa mbalimbali kusudi kazi yangu ya mbele au ya sasa isipotee bure.
3
Na Tito aliyesafiri pamoja nami hakulazimishwa kutahiriwa ingawa alikuwa Mugriki,
4
ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.
5
Lakini hatukukubali kuwatii watu wale hata kidogo, kusudi ukweli wa Habari Njema uendelee kuchungwa kati yenu siku zote.
6
Lakini kuelekea wale waliohesabiwa kuwa waongozi, hainifalii kitu kujua cheo gani walichokuwa nacho, kwa maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya inje. Watu wale hawakunifundisha kitu kipya.
7
Lakini walitambua kuwa Mungu amenipatia kazi ya kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine sawa alivyomupatia Petro kazi ya kuihubiri kwa Wayuda.
8
Kwa maana yule aliyemuwezesha Petro kuwa mutume kwa Wayuda, ndiye aliyeniwezesha vilevile kuwa mutume kwa watu wa mataifa mengine.
9
Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.
10
Lakini kitu kimoja walichotuomba ni kukumbuka wamasikini wa makanisa yao, nami nimefanya vile kwa bidii.
11
Petro alipofika Antiokia, nilibishana naye waziwazi, kwa sababu alikuwa akidanganyika.
12
Kwa maana mbele ya kufika kwa watu wamoja waliotumwa na Yakobo kule, yeye alizoea kula pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini watu wale walipofika, akajitenga na kuacha kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa sababu ya kuogopa wale wanaolazimisha kutahiriwa.
13
Na waamini wengine Wayuda wakaanza kutenda kwa unafiki sawa Petro, na hata Barnaba akajiunga nao katika huo unafiki wao.
14
Wakati nilipoona kwamba walikuwa wakitembea kinyume cha ukweli wa Habari Njema, nikamwambia Petro hivi mbele ya watu wote: “Ikiwa wewe unayekuwa Muyuda unafuata desturi za watu wa mataifa mengine, namna gani unaweza kuwalazimisha watu wa mataifa mengine wafuate desturi za Wayuda?”
15
Hakika sisi Wayuda wa kizalikio hatuko watu wa mataifa mengine, hao wenye zambi.
16
Lakini, tunajua kwamba mutu hahesabiwi haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, lakini kwa njia ya kuamini Yesu Kristo. Sisi vilevile tumeamini Yesu Kristo kusudi tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika yeye, wala si kwa njia ya kushika Sheria. Ni vile kwa maana hakuna mutu atakayehesabiwa haki kwa njia ya kushika Sheria.
17
Sasa tunapotafuta kuhesabiwa haki katika kuungana na Kristo, inaonekana kwamba sisi nasi ni wenye zambi sawa watu wa mataifa mengine. Jambo hili linaonyesha ya kama Kristo anatumika kwa ajili ya kuendelesha zambi? Hapana hata kidogo!
18
Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha kubomoa, basi ninahakikisha kwamba mimi nimevunja Sheria.
19
Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.
20
Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.
21
Mimi sitaki kukataa neema ya Mungu kwa maana ikiwa wanaweza kuhesabiwa haki mbele ya Mungu, kwa njia ya kushika Sheria, basi Kristo alikufa bure.
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 3 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6