bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Galatians 6
Galatians 6
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
1
Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.
2
Musaidiane ninyi kubeba mizigo yenu, na hivi mutatimiza sheria ya Kristo.
3
Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.
4
Kila mutu achunguze mwenendo wake mwenyewe. Basi akiwa na sababu ya kujivuna, ajivune kufuatana na mwenendo wake mwenyewe pasipo kujilinganisha na mutu mwingine.
5
Kwa maana kila mutu anapaswa kubeba muzigo wake mwenyewe.
6
Mwenye kufundishwa Habari Njema anapaswa kushirikiana mapato yake na yule anayemufundisha.
7
Musidanganyike: Mungu hachekelewi. Chochote mutu atakachopanda, ndicho atakachovuna.
8
Anayepanda kwa kupendeza hali yake ya kimwili, atavuna matunda yanayotokana na hali ile, nayo ni lufu. Lakini anayepanda kwa kupendeza Roho Mutakatifu, atavuna matunda yanayotokana na Roho yule, nayo ni uzima wa milele.
9
Tusichoke kutenda mema; kwa maana siku zitakapotimia tutavuna kama tusiporegea.
10
Basi, tunapokuwa bado na wakati, tufanye mema kwa watu wote, na zaidi kwa wandugu zetu katika imani.
11
Mujionee wenyewe ni kwa herufi kubwa gani nimewaandikia ninyi kwa mukono wangu mwenyewe!
12
Wale watu wanaowalazimisha ninyi kutahiriwa, ndio wanaotaka kujionyesha katika mambo yanayoelekea mwili. Lakini wanafanya vile tu kusudi wasiteswe kwa ajili ya kuhubiri habari za musalaba wa Kristo.
13
Watu hao wanaotahiriwa, hawashiki Sheria lakini wanataka mutahiriwe kusudi wapate kujivuna kwamba wanawashurutisha kuwa na kitambulisho kile juu ya mwili wenu.
14
Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.
15
Kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu; kitu cha lazima ni kuwa kiumbe kipya.
16
Na wote wanaofuata kanuni hii katika maisha yao pamoja na watu wa Mungu wanaohesabiwa kama Waisraeli wa kweli, ninawatakia amani na wema.
17
Basi sasa, mutu asinisumbue tena kwa maana niko na makovu juu ya mwili wangu niliyopata kwa ajili ya Yesu.
18
Wandugu, ninawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Amina.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
All chapters:
1
2
3
4
5
6