bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Galatians 5
Galatians 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 6 →
1
Kristo ametukomboa katika utumwa kusudi tukuwe huru kabisa. Basi, musimame imara wala musijitie tena katika vifungo vya utumwa.
2
Musikilize! Mimi Paulo ninataka kuwaambia kwamba kama mukikubali kutahiriwa, Kristo hana mafaa yoyote kwenu.
3
Mimi ninasema tena wazi, kila mutu anayekubali kutahiriwa sherti ashike Sheria yote.
4
Kama munatafuta kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, mumejitenga mbali na Kristo na kujipotezea neema ya Mungu.
5
Lakini sisi tunangojea kwa matumaini kwamba kwa uwezo wa Roho, tutahesabiwa haki kwa njia ya imani.
6
Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.
7
Ninyi mulikuwa na mwenendo muzuri! Ni nani aliyewazuiza kushika ukweli?
8
Kishawishi hicho hakikutoka kwa Mungu anayewaita ninyi kuwa watu wake.
9
“Chachu kidogo inachachisha donge zima.”
10
Ingawa vile mimi niko na tumaini juu yenu kutoka kwa Bwana kwamba hamutakuwa na nia mbalimbali na mimi. Lakini yule anayewavuruga ataazibiwa hata ikiwa ni nani.
11
Wandugu, ikiwa mimi ningali ninahubiri ya kama ni lazima kutahiriwa, basi kwa sababu gani ningali ninateswa? Kama ningefanya vile, basi watu hawangechukizwa na mahubiri yangu juu ya musalaba wa Kristo.
12
Heri wale wanaoleta fujo kati yenu wangejikata viungo vyao vya uzazi.
13
Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.
14
Kwa maana Sheria yote inafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.”
15
Lakini kama mukiumana na kukulana kama nyama wa pori, muangalie vizuri musiteketezane.
16
Mambo ninayotaka kusema ni haya: muishi chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu, nanyi musitimize tamaa za kimwili.
17
Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.
18
Lakini kama mukiongozwa na Roho Mutakatifu, hamutaishi tena chini ya Sheria.
19
Matendo ya kimwili yanajulikana wazi, nayo ndiyo uasherati, uchafu, kutawaliwa na tamaa za kimwili,
20
kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,
21
chuki, uuaji, ulevi, ulafi, na mambo mengine yanayofanana na hayo. Ninawaonya tena kama vile nilivyowaonya mbele, kwamba watu wanaotenda mambo kama hayo hawatashiriki katika Ufalme wa Mungu.
22
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,
23
upole na kujizuiza. Hakuna Sheria inayokataza mambo kama hayo!
24
Nao watu wa Kristo Yesu wameua hali yao ya kimutu pamoja na vifungo vyao vyote na tamaa zote mbaya.
25
Kufuatana na vile tunavyoishi kwa nguvu za Roho, basi tufuate maongozi ya Roho vilevile.
26
Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 6 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6