bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Genesis 23
Genesis 23
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 24 →
1
Sara aliishi miaka mia moja makumi mbili na saba. Hiyo ndiyo iliyokuwa miaka ya maisha ya Sara.
2
Alikufia kule Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana. Abrahamu akaomboleza na kumufanyia Sara muke wake kilio.
3
Abrahamu akaacha maiti ya muke wake, akatoka na kwenda kuzungumuza na Wahiti, akawaambia:
4
“Mimi ninaishi kama mugeni kati yenu. Munipatie sehemu ya udongo ya kaburi, kusudi nipate kumuzika marehemu muke wangu.”
5
Wahiti wakamujibu:
6
“Ee bwana wetu, usikilize; wewe ni kiongozi mukubwa kati yetu. Umuzike marehemu muke wako katika kaburi lolote utakalojichagulia; hakuna yeyote kati yetu atakayekunyima kaburi lake, wala kukuzuia kumuzika marehemu muke wako.”
7
Kisha Abrahamu akasimama na kuinama kwa heshima mbele ya wanainchi Wahiti,
8
akawaambia: “Ikiwa munaniruhusu nimuzike marehemu muke wangu, tafazali mumwombe Efuroni mwana wa Sohari, kwa ajili yangu,
9
aniuzishie lile pango lake la Makipela linalokuwa kwa mupaka wa shamba lake. Mumusihi aniuzishie nilifanye makaburi yangu. Anipatie kwa bei ya haki hapahapa mbele yenu.”
10
Efuroni mwenyewe alikuwa kati ya Wahiti hao waliokuwa wamekutanika kwenye mulango wa muji. Basi, Efuroni Muhiti, akamujibu Abrahamu mbele ya Wahiti wote pale kwenye mulango:
11
“Hapana bwana. Tafazali unisikilize. Ninakupa shamba lote na pango linalokuwa mule; tena ninakupa mbele ya wanainchi wenzangu. Umuzike mule marehemu muke wako.”
12
Abrahamu akainama tena kwa heshima mbele ya wanainchi,
13
akamwambia Efuroni, wanainchi wote wakisikia: “Ninakuomba, tafazali unisikilize. Nitakulipa bei kamili ya shamba lako, na ninakuomba upokee malipo haya kusudi nipate kumuzika mule marehemu muke wangu.”
14
Efuroni akamujibu Abrahamu:
15
“Bwana, unisikilize. Shamba lenye bei ya vikoroti mia ine tu za feza ni nini kati yako na mimi? Umuzike marehemu muke wako.”
16
Abrahamu akakubaliana na Efuroni, akamupimia kadiri ya feza alizotaja mbele ya Wahiti wote, feza vikoroti mia ine, kadiri ya vipimo vya wachuuzi wa wakati ule.
17
Basi, shamba la Efuroni linalokuwa kule Makipela, upande wa mashariki ya Mamure, pango na miti yote iliyokuwa kule pamoja na eneo zima, likakuwa la
18
Abrahamu mbele ya Wahiti wote waliokutanika kwa mulango wa muji.
19
Nyuma ya hayo, Abrahamu akamuzika Sara muke wake katika pango lile lililokuwa mule katika shamba la Makipela, upande wa mashariki ya Mamure, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana.
20
Shamba na pango lililokuwa mule lililohakikishwa na Wahiti likuwe mali ya Abrahamu apate kuzika wafu wake mule.
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 24 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50