bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Genesis 46
Genesis 46
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 45
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 47 →
1
Basi, Israeli akaanza safari yake pamoja na mali yake yote. Alipofika Beri-Seba, akatoa sadaka kwa Mungu wa baba yake Isaka.
2
Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”
3
Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri. Utakapokuwa kule, nitakufanya kuwa taifa kubwa.
4
Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe kule Misri na kukurudisha huku. Utakapokufa, mukono wa Yosefu ndio utakaofumba macho yako.”
5
Basi, Yakobo akaondoka Beri-Seba. Wana wake wakamupeleka yeye, watoto wao wachanga pamoja na wake zao katika magari ambayo mufalme wa Misri alituma kwa kumubeba.
6
Walipeleka vilevile nyama na mali yao yote waliyokuwa wamechuma katika inchi ya Kanana, wakakwenda Misri. Yakobo aliwapeleka wazao wake wote:
7
wana wake, wajukuu wake wanaume na wanawake. Wote akawaleta Misri.
8
Hawa ndio wazao wa Israeli ambao walikwenda Misri pamoja naye: Rubeni, muzaliwa wake wa kwanza,
9
pamoja na wana wa Rubeni: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi.
10
Simeoni na wana wake: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Sauli, aliyezaliwa kwa mwanamuke Mukanana.
11
Lawi na wana wake: Gersoni, Kohati na Merari.
12
Yuda na wana wake: Eri, Onani, Sela, Peresi na Zera. (Lakini Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanana). Wana wa Peresi walikuwa Hesironi na Hamuli.
13
Isakari na wana wake: Tola, Puwa, Yasubu na Simuroni.
14
Zebuluni na wana wake: Seredi, Eloni na Yaleli.
15
Hao ndio wana ambao Lea alimuzalia Yakobo kule Padani-Aramu, pamoja na Dina binti yake. Jumla ya wana wake, wabinti zake na wajukuu wake walikuwa watu makumi tatu na watatu.
16
Gadi na wana wake: Sifioni, Hagi, Suni, Esiboni, Eri, Arodi na Areli.
17
Aseri na wana wake: Imuna, Isiwa, Isiwi, Beria na Sera, dada yao. Beria na wana wake: Heberi na Malkieli.
18
Hawa kumi na sita ni wazao wa Yakobo na Zilpa, mujakazi ambaye Labani alimupa binti yake Lea.
19
Rakeli alimuzalia Yakobo wana wawili: Yosefu na Benjamina.
20
Kule Misri, Asenati binti ya Potifera, aliyekuwa kuhani wa muji wa Oni, alimuzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efuraimu.
21
Wana wa Benjamina walikuwa Bela, Bekeri, Asibeli, Gera, Namani, Ehi, Rosi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
22
Watu hao kumi na wane ni wazao wa Yakobo na muke wake Rakeli.
23
Dani na mwana wake Husimu.
24
Nafutali na wana wake: Yaseli, Guni, Yeseri na Silemu.
25
Hao saba ni wazao wa Yakobo na Biliha, mujakazi ambaye Labani alimupa binti yake Rakeli.
26
Jumla ya wazao wa Yakobo aliokwenda nao Misri, bila kuwahesabu wake za wana wake, ilikuwa watu makumi sita na sita.
27
Kule katika inchi ya Misri Yosefu alikuwa amepata wana wawili. Kwa hiyo watu wote wa jamaa ya Yakobo walioingia Misri walikuwa makumi saba.
28
Yakobo akamutanguliza Yuda kwa Yosefu kumwomba waonane kule Goseni. Nao wakafika katika eneo la Goseni.
29
Yosefu akapanda gari lake la farasi, akakwenda kumupokea baba yake Israeli, kule Goseni. Alipomufikia baba yake, alimukumbatia na kulia kwa kitambo kirefu.
30
Israeli akamwambia Yosefu: “Hata nikikufa sasa si kitu kwa sababu nimeuona uso wako na kujua kwamba wewe uko muzima!”
31
Yosefu akawaambia wandugu zake na jamaa yote ya baba yake: “Ninakwenda kumwarifu mufalme wa Misri kwamba wandugu zangu na jamaa yote ya baba yangu waliokuwa katika inchi ya Kanana wamekuja kwangu.
32
Nitamwelezea kwamba ninyi ni wachungaji maana mumekuwa mukichunga nyama, na kwamba mumefika pamoja na mbuzi, kondoo, ngombe na mali yenu yote.
33
Basi, mufalme akiwaita na kuwauliza: ‘Kazi yenu ni nini?’
34
Museme: ‘Bwana, sisi watumishi wako, ni wafugaji wa nyama tangu utoto wetu mpaka leo, maana ndivyo babu zetu walivyokuwa.’ Museme hivyo kusudi muruhusiwe kukaa katika eneo la Goseni.” Yosefu alisema hivyo kwa sababu kwa Wamisri wachungaji wote wa kondoo ni chukizo.
← Chapter 45
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 47 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50