bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Genesis 35
Genesis 35
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 34
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 36 →
1
Siku moja, Mungu akamwambia Yakobo: “Anza safari, uende kuishi Beteli na kunijengea mazabahu kule, mimi Mungu niliyekutokea wakati ulipomukimbia kaka yako Esau.”
2
Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.
3
Kisha, tutakwenda Beteli kusudi nimujengee Mungu mazabahu, Mungu ambaye alinisaidia siku ya taabu na kuwa nami popote nilipokwenda.”
4
Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.
5
Yakobo na wana wake walipokuwa wakisafiri, Mungu akawatia hofu wenyeji wa miji yote ya jirani hata hawakusubutu kuwafuatilia.
6
Basi, Yakobo akafika Luzi, maana yake Beteli, katika inchi ya Kanana, pamoja na watu wote aliokuwa nao.
7
Akajenga mazabahu pahali pale na kupaita “Mungu wa Beteli” maana ni pale ndipo pahali Mungu alipojionyesha kwake wakati alipokuwa akimukimbia kaka yake.
8
Debora, mulezi wa Rebeka, akakufa, akazikwa chini ya muti wa mwalo upande wa kusini wa Beteli. Kwa hiyo Yakobo akauita muji ule “Mwalo wa Maombolezo”.
9
Wakati alipokuwa akirudi kutoka Padani-Aramu, Mungu akamutokea tena Yakobo na kumubariki.
10
Mungu akamwambia: “Jina lako ni Yakobo, lakini hautaitwa hivyo tena, lakini sasa jina lako litakuwa Israeli.” Kwa hiyo Yakobo akaitwa Israeli.
11
Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.
12
Inchi niliyowapa Abrahamu na Isaka nitakupa wewe na wazao wako.”
13
Basi, nyuma ya kuongea na Yakobo, Mungu akamwacha na kupanda juu.
14
Yakobo akasimika nguzo ya jiwe la ukumbusho pahali pale Mungu alipozungumuza naye, akaitakasa kwa kuimiminia sadaka ya kinywaji na mafuta.
15
Basi, Yakobo akapaita pahali pale alipozungumuza na Mungu Beteli.
16
Yakobo na jamaa yake yote wakaendelea na safari yao kutoka Beteli. Walipokuwa umbali fulani mbele ya kufika Efurata, Rakeli akashikwa na uchungu mukali wa kuzaa.
17
Naye alipokuwa katika uchungu ule, muzalishaji akamwambia: “Usiogope, umepata mutoto mwingine mwanaume.”
18
Rakeli akiwa karibu kufa, akamupa yule mutoto jina Beni-oni. Lakini baba yake akamwita mutoto yule Benjamina.
19
Basi, Rakeli akakufa na kuzikwa kando ya njia inayokwenda Efurata, ni kusema Betelehemu.
20
Yakobo akasimika nguzo ya ukumbusho juu ya kaburi ya Rakeli ambayo iko mpaka leo.
21
Israeli, ndiye Yakobo, akaendelea na safari yake na kupiga kambi yake ngambo ya munara wa Ederi.
22
Wakati Israeli alipokuwa anakaa katika inchi ile, mwana wake Rubeni, akalala na Biliha, habara ya baba yake. Naye Israeli akasikia habari hizo. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili.
23
Wana wa Lea walikuwa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuluni.
24
Wana wa Rakeli walikuwa Yosefu na Benjamina.
25
Wana waliozaliwa na Biliha, mujakazi wa Rakeli, walikuwa Dani na Nafutali.
26
Na wana waliozaliwa na Zilpa, mujakazi wa Lea, walikuwa Gadi na Aseri. Hao ndio wana wa Yakobo, aliozaa alipokuwa kule Padani-Aramu.
27
Yakobo akaondoka akakwenda Mamure kwa baba yake Isaka, kule Kiriati-Arba ni kusema Hebroni, pahali ambapo Abrahamu na Isaka walikaa kama wageni.
28
Isaka alipokuwa na miaka mia moja na makumi nane,
29
akiwa muzee wa miaka mingi, akakufa na kukutana na wazee wake. Watoto wake, Esau na Yakobo wakamuzika.
← Chapter 34
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 36 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50