bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Genesis 38
Genesis 38
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 37
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 39 →
1
Wakati ule, Yuda akatengana na wandugu zake, akakwenda kukaa na mutu mumoja Mwadulami, jina lake Hira.
2
Akiwa kule, Yuda akamwona binti ya Sua Mukanana, akamwoa.
3
Binti ya Sua akapata mimba akazaa mutoto mwanaume, akamwita Eri.
4
Akapata mimba ingine, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Onani.
5
Kisha akapata mutoto mwingine mwanamuke, akamwita Sela. Wakati Sela alipozaliwa, Yuda alikuwa Kezibu.
6
Yuda alimwoea mutoto wake wa kwanza Eri mwanamuke anayeitwa Tamari.
7
Lakini Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Yawe, hivyo Yawe akamwua.
8
Basi, Yuda akamwambia Onani: “Umutwae muke wa ndugu yako marehemu, maana vile ndivyo inavyokupasa kufanya, upate kumuzalia ndugu yako watoto.”
9
Lakini Onani alijua kwamba hao watoto hawangekuwa wake. Kwa hiyo, alipolala na muke wa ndugu yake, alimwanga chini mbegu ya uzazi, kusudi asimupatie ndugu yake watoto.
10
Tendo hilo likamwuzi Yawe, akamwua Onani vilevile.
11
Halafu Yuda akamwambia Tamari, muke wa mwana wake: “Rudi kwa nyumba ya baba yako, ubaki mujane mpaka wakati mwana wangu Sela atakapokomaa.” Yuda hakutaka Sela naye akufe kama vile wandugu zake. Basi, Tamari akarudi kwa nyumba ya baba yake.
12
Nyuma ya muda, binti ya Sua, muke wa Yuda, akakufa. Yuda alipomaliza kufanya kilio akaondoka na rafiki yake Hira Mwadulami, wakakwenda Timuna kwa kukata manyoya ya kondoo wake.
13
Tamari aliposikia kwamba baba mukwe wake alikuwa katika njia kwenda Timuna kukata manyoya ya kondoo wake,
14
akavua nguo zake za ujane na kujifunika kitambaa. Kisha akaikaa kwenye mulango wa kuingilia Enaimu, kijiji kilichokuwa katika njia kwenda Timuna. Alifanya hivyo kwa vile aliona kwamba Sela alikwisha kuwa mutu muzima, lakini yeye Tamari hakuoeshwa akuwe muke wake.
15
Basi, Yuda alipokuta Tamari pale, alimuzania kuwa mwanamuke kahaba, maana alikuwa akijifunika uso.
16
Halafu, bila kujua kwamba huyo alikuwa muke wa mwana wake, akamwendea pale kando ya njia, akamwambia: “Ninataka kulala nawe.” Tamari akamwuliza: “Utanipa nini upate kulala nami?”
17
Yuda akamujibu: “Nitakupa mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Tamari akamwambia: “Weka rehani kwa kuhakikisha kwamba utaniletea yule mwana-mbuzi.”
18
Yuda akamwuliza: “Unataka nikupe nini kama rehani?” Naye akamujibu: “Unipe hiyo pete na kamba yake pamoja na hiyo fimbo unayoshika.” Basi, Yuda akamupa vitu hivyo vyote, akalala naye. Tamari akapata mimba yake.
19
Basi, Tamari akarudi kwa nyumba akavua kile kitambaa alichojifunika, akavaa tena nguo zake za ujane.
20
Wakati Yuda alipomutuma yule rafiki yake, Mwadulami, amupelekee yule mwanamuke mwana-mbuzi kusudi arudishiwe rehani aliyomwachia, Hira hakumupata.
21
Hira akauliza wenyeji wa Enaimu: “Yuko wapi yule mwanamuke kahaba aliyekuwa kando ya njia karibu na hapa?” Wakamujibu: “Hapa hapajakuwa mwanamuke kahaba.”
22
Basi, huyo rafiki akarudi kwa Yuda, akamwambia: “Sikumupata! Tena wenyeji wa kule wameniambia kwamba hapajakuwa mwanamuke kahaba yeyote kule.”
23
Yuda akasema: “Acha avichukue vitu hivyo. Kama sivyo atatufanya tuchekelewe. Wewe mwenyewe umeona kwamba nilimupelekea mwana-mbuzi, lakini wewe haukumupata.”
24
Kisha miezi mitatu, Yuda akapata habari hii: “Tamari, muke wa mwana wako amekuwa kahaba, tena amepata mimba kwa kufanya ukahaba.” Basi, Yuda akaamuru: “Mumutoshe inje achomwe kwa moto!”
25
Walipokuwa wakimutoa inje, Tamari akatuma ujumbe kwa baba mukwe wake, akisema: “Mwenye vitu hivi ndiye aliyenipa mimba. Kwa hiyo, ninakuomba umutambue mwenye pete hii na kamba yake, na fimbo hii.”
26
Yuda akavitambua vitu hivyo, akasema: “Tamari ni mwenye haki kuliko mimi. Ni kweli, maana sikumwoesha kwa mwana wangu Sela.” Tokea siku hiyo Yuda hakulala tena na Tamari.
27
Wakati wa kuzaa kwa Tamari ulipofika, ikafahamika kwamba alikuwa na mimba ya mapacha.
28
Basi, alipopata uchungu wa kuzaa, pacha mumoja akatoa mukono inje, naye muzalishaji akaufunga kwa uzi mwekundu, akisema: “Huyu ndiye aliyezaliwa kwanza.”
29
Lakini yule mutoto alipourudisha mukono wake ndani, ndugu yake akazaliwa wa kwanza. Muzalishaji akasema: “Mbona wewe umepita kwa nguvu?” Kwa hiyo akaitwa Peresi.
30
Kisha ndugu yake akazaliwa akiwa na ule uzi mwekundu kwenye mukono, naye akaitwa Zera.
← Chapter 37
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 39 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50