bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
/
Job 18
Job 18
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 19 →
1
Bildadi Mshuhi akajibu:
2
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6
Mwanga kwenye hema lake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; hila zake mwenyewe zinamwangusha.
8
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14
Atang’olewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 19 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42