bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
/
Micah 6
Micah 6
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 7 →
1
Yasikieni, Bwana anayoyasema: Haya! Bisheni mbele ya milima, vilima vizisikie sauti zenu!
2
Ninyi milima, yasikieni masuto ya Bwana! Yasikieni nanyi miamba mlio misingi ya nchi! Kwani Bwana ana shauri nao walio ukoo wake, hana budi kuumbuana na Waisiraeli!
3
Ninyi mlio ukoo wangu, nimewafanyizia nini? Nimewachokoza kwa nini? Nijibuni!
4
Kwani niliwatoa katika nchi ya Misri, nikawaleta huku, nikawakomboa katika nyumba, mlimokuwa watumwa, nikamtuma Mose na Haroni na Miryamu, wawatangulie.
5
Mlio ukoo wangu, yakumbukeni, Balaka, mfalme wa Moabu, aliyowawazia, nayo Bileamu, mwana wa Beori, aliyomjibu! Yakumbukeni nayo yaliyofanyika toka Sitimu mpaka Gilgali, mpate kujua, ya kuwa Bwana ni mwongofu.
6
Nimtokee Bwana na kumpa nini nikimnyenyekea Mungu Alioko huko juu? nimtolee ng'ombe za tambiko za kuteketezwa nzima, kama ndama za mwaka mmoja
7
Je? Bwana atapendezwa na maelfu ya madume ya kondoo? Au atapendezwa na maelfu kumi ya vijito vya mafuta? Au nimpe mwanangu wa kwanza, awe ng'ombe ya tambiko ya kuondolea mapotovu yangu? Je? Zao la tumbo langu liyalipe makosa ya roho yangu?
8
Umeambiwa, wewe mtu, yaliyo mema, nayo Bwana anayoyatafuta kwako: Yafanye yapasayo ukipenda kuwahurumia wenzako, tena ukiendelea kushikamana na Mungu wako na kujinyenyekeza.
9
Sauti ya Bwana inawaita waliomo mjini, - nako kulitazamia Jina lako ni ujuzi - inasema: Isikieni fimbo iwapigayo! Msikieni naye aliyeiagiza!
10
Je? Nyumbani mwao wasiomcha Mungu yangalimo bado malimbiko yaliyopatwa kwa uovu? nazo zile pishi nyembamba zilizoapizwa?
11
Niwawazie kuwa wametakata, ijapo watumie mizani za kuchukulia mali za watu bure? au ijapo watie mishipini vijiwe vya kupimia vidanganyavyo watu?
12
Matajiri ya kwao huzidi ukorofi, nao wenyeji wao husema uwongo, nazo ndimi zao vinywani mwao hudanganya watu.
13
Kwa hiyo nami nitakupiga, usipone; nitakuangamiza kwa ajili ya makosa yako.
14
Wewe utakula, lakini hutashiba, njaa ikae tumboni mwako. Utakayoyapeleka pengine hutayaponya; nayo utakayoyaponya, nitayatolea panga.
15
Wewe utapanda, lakini hutavuna; wewe utakamua chekele, lakini hutajipaka mafuta; utakamua zabibu, lakini hutakunywa mvinyo.
16
Kwani mmeyashika maongozi ya Omuri, mkayafanya matendo yote ya mlango wa Ahabu, mkayafuata mashauri yao, niigeuze nchi yenu, iwe mapori matupu, nao watakaokaa huku wazomelewe. Hivyo ndivyo, mtakavyotwikwa matusi yao walio ukoo wangu.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7