bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Chronicles 11
1 Chronicles 11
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 12 →
1
Kisha Waisraeli wote walikusanyika mbele ya Daudi kule Hebroni, wakamwambia: “Sisi ni mwili na damu yako.
2
Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe, Mungu wako alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli, na utakuwa mukubwa wa watu wangu Waisraeli.’ ”
3
Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme kule Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Waisraeli kulingana na neno la Yawe lililotolewa kwa njia ya Samweli.
4
Nyuma ya hayo Daudi na Waisraeli wote walikwenda Yerusalema, muji uliojulikana kwa jina la Yebusi, na ambao wenyeji wake walikuwa Wayebusi.
5
Wakaaji wa Yebusi wakamwambia Daudi: “Hautaingia katika muji huu.” Hata hivyo, Daudi akanyanganya makimbilio ya Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.
6
Halafu Daudi akasema: “Mutu atakayetangulia kuwapiga Wayebusi, atakuwa mukubwa na jemadari katika jeshi.” Basi Yoabu mwana wa Zeruya, akakuwa wa kwanza kuwashambulia, hivyo akakuwa mukubwa.
7
Daudi alikaa katika makimbilio yale, na kwa hiyo, muji ule ukaitwa “Muji wa Daudi.”
8
Akajenga muji ule, akianzia uwanja wa Milo, na kuuzunguka wote, na Yoabu akatengeneza muji ule upya.
9
Naye Daudi akazidi kuwa mukubwa kwa sababu Yawe wa majeshi alikuwa pamoja naye.
10
Haya ndiyo majina ya wakubwa wa mashujaa wa Daudi, ambao pamoja na watu wengine wote wa Israeli, walimwunga mukono kwa pamoja kusudi akuwe mufalme, sawa na neno Yawe alilotoa juu ya Waisraeli.
11
Haya ndiyo majina ya mashujaa wale wa Daudi: Yasobeamu, wa ukoo wa Hakemoni, aliyekuwa kiongozi wa “Wale makumi tatu.” Yeye alipigana kwa mukuki wake akaua watu mia tatu kwa mara moja katika vita.
12
Halafu aliyefuata kati ya wale mashujaa watatu alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, wa ukoo wa Ahoa.
13
Siku moja Eleazari alikuwa pamoja na Daudi kule Pasi-Damimu, wakati Wafilistini walipokusanyika kupigana vita. Kule kulikuwa shamba lenye shayiri tele, lakini Waisraeli wakawakimbia Wafilistini.
14
Lakini wakasimama imara katikati ya shamba lile kwa kulikinga, wakaua Wafilistini; Yawe akawaokoa kwa kuwapa ushindi mukubwa.
15
Kisha mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu wakamwendea Daudi kwenye mulima wa pango la Adulamu. Wakati ule jeshi la Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.
16
Naye Daudi wakati ule alikuwa katika maficho, nalo jeshi la Wafilistini lilikuwa katika muji wa Betelehemu.
17
Daudi akapatwa na hamu kubwa akasema: “Heri kama mutu angeweza kunipa maji ya kunywa kutoka katika kisima cha Betelehemu kinachokuwa karibu na mulango wa muji!”
18
Wale mashujaa wake watatu wakatoka, wakapenya katikati ya kambi ya jeshi la Wafilistini, wakaenda na kuchota maji katika kisima cha Betelehemu, karibu na mulango wa muji, wakamuletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyakunywa, na kwa pahali pake akayamwanga chini kama sadaka kwa Yawe
19
akisema: “Tendo kama hili lipite mbali nami; siwezi kulifanya mbele ya Mungu wangu. Basi ninaweza kunywa damu ya maisha ya watu hawa? Maana kwa kuyahatarisha maisha yao walileta maji haya.” Kwa hiyo Daudi hakukunywa maji yale. Hayo ndiyo mambo waliyotenda wale mashujaa watatu.
20
Abisai, ndugu ya Yoabu, alikuwa mukubwa wa mashujaa makumi tatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake na watu mia tatu, akawaua, akajipatia jina kati ya wale mashujaa watatu.
21
Basi, akaheshimiwa zaidi kati ya mashujaa makumi tatu, hata akakuwa jemadari wao, lakini hakukuwa shujaa kama wale mashujaa watatu.
22
Benaya mwana wa Yehoyada, kutoka muji wa Kabuseli, alikuwa askari shujaa ambaye alifanya mambo mengi ya ajabu. Aliua mashujaa wawili kutoka Moabu, na siku moja wakati wa baridi kali, akashuka na kuua simba ndani ya shimo.
23
Vilevile, akamwua Mumisri mumoja, urefu wake ulikuwa metre mbili na nusu, naye alikuwa akibeba mukuki mukubwa sana katika mukono wake, kama muti wa mufumaji wa nguo. Lakini Benaya akamushambulia akiwa na fimbo tu, akamunyanganya mukuki ule, na kumwua Mumisri yule kwa mukuki wake mwenyewe.
24
Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, akajipatia sifa kati ya wale mashujaa watatu.
25
Basi, akakuwa mwenye heshima kati ya wale mashujaa makumi tatu, ingawa hakukuwa shujaa kama wale mashujaa watatu. Na Daudi akamupa cheo cha mukubwa wa walinzi wake wa kipekee.
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 12 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29