bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Chronicles 17
1 Chronicles 17
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 18 →
1
Wakati mufalme Daudi alipokuwa akiikaa katika nyumba yake ya kifalme, siku moja akamwita nabii Natani, na kumwambia: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba nzuri iliyojengwa na miti ya mwerezi, lakini Sanduku la Agano la Yawe linakaa ndani ya hema.”
2
Natani akamwambia Daudi: “Ufanye chochote unachofikiri ndani ya moyo wako, maana Mungu yuko pamoja nawe.”
3
Lakini usiku uleule, neno la Yawe lilimufikia Natani kusema hivi:
4
“Kwenda umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe anasema hivi: Wewe hautanijengea nyumba ya kukaa.
5
Tangu wakati ule nilipowaongoza watu wa Israeli kutoka Misri mpaka hivi leo, sijaishi katika nyumba. Nimekuwa nikihama toka hema hata hema, na toka makao hata makao mengine.
6
Kila pahali nilipokwenda na Waisraeli, sikupata hata mara moja kuwauliza waamuzi wao niliowaamuru wachunge watu wangu, ‘Kwa nini haukunijengea nyumba ya mierezi?’
7
“Kwa hiyo basi, umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa katika shamba la malisho ulipokuwa unachunga kondoo, kusudi ukuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.
8
Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye heshima kama vile wakubwa wengine wa dunia.
9
Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli pahali pa kuishi niwapandikize, kusudi waishi pahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakali wanaotumia nguvu hawatawatesa tena kama zamani,
10
wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Mimi nitawashinda waadui zako wote. Zaidi ya yote, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakupa wazao.
11
Siku zako zitakapotimia za kujiunga na babu zako, nitamufanya mumoja wa watoto wako wewe mwenyewe akuwe mufalme; nami nitaimarisha ufalme wake.
12
Yeye ndiye atakayenijengea nyumba; nami nitahakikisha kwamba ufalme wake unadumu milele.
13
Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu. Sitaacha kumutendea mema kama vile nilivyoacha kumutendea Saulo aliyekutangulia.
14
Lakini nitamwimarisha katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele, na kiti chake cha kifalme kitakuwa imara siku zote.”
15
Natani akamwelezea Daudi mambo hayo yote kulingana na maono hayo.
16
Kisha mufalme Daudi akaingia ndani ya hema na kuikaa mbele ya Yawe, halafu akaomba: “Mimi ni nani, ee Yawe Mungu, na nyumba yangu ni nini hata unitukuze hivi?
17
Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako, ee Mungu. Zaidi ya hayo, umenitolea ahadi juu ya vizazi vyangu vinavyokuja, ee Yawe Mungu!
18
Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi mutumishi wako, kwa kunitukuza vile? Wewe unanijua mimi mutumishi wako.
19
Ee Yawe, kwa ajili ya mutumishi wako na kwa kufuatana na moyo wako mwenyewe, umeyatenda hayo makubwa yote, kusudi hayo matendo makubwa yote yajulikane.
20
Hakuna mwingine kama wewe, ee Yawe, na yote tunayosikia yanahakikisha kwamba hakuna Mungu mwingine lakini wewe tu.
21
Tena ni watu gani katika dunia ambao wanaweza kulinganishwa na watu wako Waisraeli? Hao ndio watu peke yao Mungu wao alikwenda kuwakomboa kusudi wakuwe watu wake. Ukajipatia sifa kwa kutenda mambo makubwa na ya ajabu pale ulipofukuza mataifa mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kutoka Misri.
22
Hata ukajifanyia watu wako Waisraeli kuwa watu wako milele; nawe ee Yawe, umekuwa Mungu wao.
23
“Basi sasa, ewe Yawe, uimarishe milele neno lako ulilosema juu yangu mimi mutumishi wako na juu ya jamaa yangu.
24
Nalo jina lako litatukuzwa milele, nao watu watasema: ‘Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, ndiye Mungu juu ya Israeli!’ Na jamaa yangu, mimi Daudi mutumishi wako, itaimarishwa mbele yako.
25
Maana, ee Mungu wangu, nimepata bidii ya kukuomba kwa sababu umenifunulia ukisema kwamba utanipa wazao.
26
Sasa ee Yawe, wewe ndiwe Mungu, umeniahidi mimi mutumishi wako jambo hili jema.
27
Kwa hiyo ninakuomba ubariki wazao wangu, mimi mutumishi wako, kusudi wadumu milele mbele yako; maana unapobariki, baraka zako zinadumu milele.”
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 18 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29