bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Chronicles 23
1 Chronicles 23
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 24 →
1
Daudi alipokuwa muzee wa miaka mingi, akamuweka Solomono mwana wake kuwa mufalme wa Israeli.
2
Mufalme Daudi akawakusanya wakubwa wote wa Israeli, makuhani na Walawi.
3
Walawi wote wanaume wenye umri wa miaka makumi tatu na zaidi, wakahesabiwa. Jumla yao ilikuwa elfu makumi tatu na nane.
4
Halafu, Daudi akawagawanya: elfu makumi mbili na nane kati yao wakuwe wasimamizi wa kazi ya nyumba ya Yawe, elfu sita wakuwe wakubwa na waamuzi,
5
elfu ine wakuwe walinzi wa milango, na elfu ine wakuwe waimbaji, wakimusifu Yawe kwa ala za muziki mufalme alizotengeneza mwenyewe kwa ajili ya kazi hiyo.
6
Daudi akawagawanya Walawi katika makundi matatu kulingana na ukoo za kabila la Lawi: ukoo wa Gersoni, ukoo wa Kohati na ukoo wa Merari.
7
Wana wa Gersoni walikuwa: Ladani na Simei.
8
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli mukubwa wao, Zetamu na Yoeli.
9
Wana wa Simei walikuwa watatu: Selomoti, Hazieli na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa ukoo wa Ladani.
10
Wana wengine wane wa Simei walikuwa: Yahati, Zina, Yeusi na Beria.
11
Yahati ndiye aliyekuwa mukubwa wao, akifuatwa na Zina. Lakini Yeusi na Beria, kwa vile hawakukuwa na wana wengi, walihesabiwa kama vile ukoo mumoja.
12
Wana wa Kohati walikuwa wane: Amuramu, Isari, Hebroni na Usieli.
13
Wana wa Amuramu walikuwa: Haruni na Musa. Haruni alichaguliwa kwa kazi inayoelekea vitu vitakatifu kabisa, hata wazao wake siku zote wafukizie ubani mbele ya Yawe, wakimutumikia na kuwabariki watu katika jina la Yawe milele.
14
Lakini wana wa Musa, mutu wa Mungu wanatajwa katika kabila la Lawi.
15
Wana wa Musa walikuwa: Gersoni na Eliezeri.
16
Mukubwa kati ya wana wa Gersoni alikuwa: Sebueli.
17
Mwana wa pekee wa Eliezeri alikuwa: Rehabia. Rehabia alikuwa na wana wengi sana.
18
Mwana wa Isari alikuwa: Selomiti, kiongozi wa kabila zima.
19
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria, mukubwa wao; Amaria, wa pili; Yahazieli, wa tatu; na Yekameamu, wa ine.
20
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika mukubwa wao, na Isia wa pili.
21
Wana wa Merari walikuwa: Mali na Musi. Wana wa Mali walikuwa: Eleazari na Kisi.
22
Eleazari alikufa bila mwana, lakini wabinti tu. Wabinti wale wakaolewa na binamu zao, wana wa Kisi.
23
Wana wa Musi walikuwa watatu: Mali, Ederi na Yeremoti.
24
Hao ndio wana wa Lawi kulingana na ukoo zao. Kila mumoja wao aliyetimiza umri wa miaka makumi mbili na zaidi, aliandikishwa kwa jina, na alishiriki katika kazi ya kujenga nyumba ya Yawe.
25
Daudi akasema: “Yawe, Mungu wa Israeli, amewapa watu wake amani, naye ataishi Yerusalema kwa milele.
26
Kwa hiyo, Walawi hawatahitaji tena kubeba hema takatifu au vyombo vyake vya ibada.”
27
Kulingana na maagizo ya mwisho Daudi aliyotoa, Walawi wote waliofikia umri wa miaka makumi mbili waliandikishwa.
28
Kazi yao ilikuwa ni kuwasaidia makuhani wa ukoo wa Haruni katika kazi ya kujenga nyumba ya Yawe, kutunza viwanja na vyumba, kusafisha vyombo vitakatifu vyote na kufanya kazi zinazoelekea kujenga nyumba ya Yawe.
29
Pamoja na hayo, walisaidia katika kazi kutayarisha mikate mitakatifu, unga safi na sadaka ya vyakula, maandazi yasiyotiwa chachu, sadaka ya mikate iliyokaangwa, sadaka ya mikate iliyochanganywa na mafuta, na sadaka katika kazi ya upimaji wa wingi wa sadaka na ukubwa wake.
30
Walisimama kwa kumushukuru na kumusifu Yawe kila siku asubui na magaribi,
31
na wakati wa siku za Sabato, mwandamo wa mwezi na sikukuu zingine, pale sadaka za kuteketezwa kwa moto zilipotolewa kwa Yawe. Sheria ziliwekwa kuelekea hesabu ya Walawi walioagizwa kufanya kazi zile siku zote mbele ya Yawe.
32
Kwa hiyo, ilikuwa ni kazi yao kutunza hema la kusanyiko na Pahali Patakatifu, na kuwasaidia wandugu zao makuhani, wazao wa Haruni, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe.
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 24 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29