bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jeremiah 29
Jeremiah 29
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 28
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 30 →
1
Hii ni barua ambayo nabii Yeremia aliyotuma kutoka Yerusalema kwa wasimamizi wa watu waliopelekwa katika uhamisho Babeli pamoja na makuhani, manabii, na watu wote wengine ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kutoka Yerusalema na kuwapeleka kule.
2
Wakati huu ulikuwa nyuma ya kuondoka Yerusalema kwa mufalme Yekonia na malkia mama wa mufalme, matowashi wa mufalme, wakubwa wa inchi ya Yuda na wa Yerusalema, wafundi na wafua vyuma.
3
Barua hii ilitumwa kwa mukono wa Elasa mwana wa Safamu, na Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Zedekia mufalme wa Yuda, aliowatuma kwa Nebukadneza mufalme wa Babeli. Nayo iliandikwa hivi:
4
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya watu wote aliowatoa wapelekwe katika uhamisho kutoka Yerusalema na kwenda Babeli:
5
Mujijengee nyumba za kukaa. Mulime mashamba, mupande mbegu na kula mazao yake.
6
Muoe, mupate watoto. Muwaoee wana wenu na kuowesha wabinti zenu, nao vilevile wapate watoto. Muongezeke kule wala musipunguke.
7
Mushugulike na kuleta ustawi katika muji ule ambamo nimewahamishia. Muuombee muji huo kwa Yawe, maana ukistawi ninyi vilevile mutastawi.
8
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Musikubali kudanganywa na manabii wenu na waaguzi wanaokuwa katikati yenu, wala musisikilize ndoto wanazoota.
9
Maana wanawatabiria uongo kwa kutumia jina langu. Mimi sikuwatuma. –Ni ujumbe wa Yawe.
10
Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.
11
Maana, mimi ninajua mupango ninaokuwa nao juu yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nayo mipango yangu ni ya kuwatendea mema wala si mabaya, kusudi mupate kuwa na tumaini katika siku zinazokuja.
12
Kwa hiyo mutakapokuja kunililia na kuniomba, nitawasikiliza.
13
Mutanitafuta mimi na kuniona. Mutakaponitafuta kwa moyo wote,
14
mutaniona. Nitatengeneza upya maisha yenu na kuwakusanya kutoka mataifa yote na pahali pote nilipowasambaza. Nitawarudisha pahali nilipowaondoa wakati nilipowapeleka katika uhamisho. –Ni ujumbe wa Yawe.
15
Ninyi munasema: Yawe ametuinulia manabii huko Babeli.
16
Yawe anasema hivi juu ya mufalme anayetawala katika kiti cha kifalme cha Daudi, na juu ya watu wote wanaokaa katika muji huu, ndio wandugu zenu ambao hawakuondoka kwenda pamoja nanyi katika uhamisho:
17
Nitawatumia vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kama matunda mabaya sana ya tini zisizoweza hata kukuliwa.
18
Nitawashambulia kwa vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia; nitawafanya kuwa mufano wa kutumia kwa kutoa laana. Mutakuwa kitu cha kushangaza, cha kuzarauliwa na cha kuzomewa kati ya mataifa yote nitakapowasambaza.
19
Nitafanya hivyo kwa sababu hamukusikiliza maneno yangu niliyowaambia kila mara kwa njia ya watumishi wangu, manabii, nanyi mukakataa kusikiliza. –Ni ujumbe wa Yawe.
20
Enyi wote niliowaondoa kutoka Yerusalema na kuwapeleka katika uhamisho kule Babeli, musikilize neno langu mimi Yawe.
21
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya Ahabu, mwana wa Kolaya na juu ya Zedekia mwana wa Masea, ambao wanawatabiria uongo kwa jina lake: Nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli, naye atawaua waziwazi mbele ya macho yenu.
22
Kwa sababu jambo hilo litakalowapata, watu wote waliohamishiwa Babeli kutoka Yuda, watatumia mufano huu kwa kutoa laana: Yawe akufanye kama Zedekia na Ahabu, ambao mufalme wa Babeli aliwachoma katika moto.
23
Jambo hili litawafikia kwa sababu wametenda katika Israeli mambo yasiyofanyika. Walizini na wake za jirani zao, na kusema maneno ya uongo kwa jina langu, jambo ambalo mimi sikuwaamuru wafanye. Mimi ninajua hayo. Nimeyashuhudia. –Ni ujumbe wa Yawe.
24
Yawe akaniagiza kumwambia Semaya wa Nehelamu hivi:
25
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Umejiruhusu kutuma barua kwa wakaaji wote wa Yerusalema na kwa kuhani Zefania, mwana wa Masea na kwa makuhani wengine wote. Katika barua hiyo, ulimwambia Zefania hivi:
26
Yawe amekufanya wewe Zefania kuwa kuhani kwa pahali pa kuhani Yehoyada, kusudi ukuwe mukubwa wa nyumba ya Yawe. Wewe utashugulika na kumutia katika kifungo na kumufunga kwa minyororo mwenda-wazimu yeyote anayetabiri.
27
Kwa nini basi, haukukaripia Yeremia wa muji wa Anatoti ambaye anakutabiria?
28
Maana yeye alituma habari huko Babeli, akisema: Mutabaki katika uhamisho kwa muda murefu, mujenge nyumba za kukalia, mulime mashamba, mupande mbegu na kula mazao yake!
29
Kuhani Zefania akamusomea nabii Yeremia barua hiyo.
30
Neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
31
Utume ujumbe huu kwa watu wote wanaokuwa katika uhamisho: Yawe anasema hivi juu ya Semaya wa Nehelamu: Semaya amewatabiria ninyi ingawa mimi sikumutuma na kuwasukuma musadikie uongo.
32
Kwa hiyo nitamwazibu Semaya wa Nehelamu pamoja na wazao wake. Hakuna hata mumoja wa watu wake atakayebaki muzima na kupata kuona mema nitakayowafanyia watu wangu, kwa sababu amesema maneno ya uasi juu ya Yawe. –Ni ujumbe wa Yawe.
← Chapter 28
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 30 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52